Sunday, March 30, 2014

HABARI AMBAYO INATIKISA NCHI----KARIAKOO YAHAMIA COCO BEACH KWA MUDA,YALE MAONYESHO MAKUBWA YA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO YANAENDELEA MUDA HUU.CHUKUA MUDA WAKO KUFAIDI KINACHOENDELEA HUKO

Wateja mbalimbalia ambao habari24 blog imewanasa asubuhi ya leo jumapili wakiwa tayari wanafaya shoping zao ndani ya maonyesho hayo ambayo yanafanyika katika ufukwe wa coco beach,maonyesho ambayo yameandaliwa na kampuni ya HAZINA CAPITALlakini kupata udhamini mkubwa wa mtandao wa TIGO TANZANIA

Bidhaa ambazo huwa unazipata ndani ya soko la kariakoo sasa zinapatikana ndani ya ufukwe wa coco beach kwa gharama nafuu sana na bidhaa nzuri kwa utulivu kabisa


wauzaji wa bidhaa hizo wakiwa wanaweka mambo sawa asubuhi hii wakati wakijiandaa kuwahudumia mamia ya wateja wa dar es salaam watakaojaa muda sio mrefu ndani ya coco beach
Maonyesho hayo yameanza jana jumamosi na yatamalizika leo jumapili huku yakiwajia tena wikiend nyingine ya mwisho wa mwezi

Ukifika eneo hili burudani za music mchanganyiko pia zipo kwa wingi sana
Mabanda mbali mbali ya wafanyabiashara yakiwa tayari kabisa kama yalivyonaswa na mwandishi wa mtandao huu mapema asubuhi ya jumapili ya leo
Waandishi wa habari mbalimbali wakizungumza na wafanyabiashara hao ambao wamekiri kuwa biashara zinaenda vizuri na wateja wanakuja kwa wingi hasa majira ya jioni hivyo kuwashukuru kampuni ya tigo na HAZINA CAPITAL kwa kuwapa fursa hiyo ya kufanya biashara zao katika fukwe hizo
Muonekano wa maonyesho hayo kwa nje
Kwa mujibu wa waandaaji wa maonyesho hayo ni kuwa maonyesho hayo yatakuwa yanafanyika kila wikiend ya mwisho wa mwezi ambapo yanawashirikisha wafanyabiashara mbalimbali kutoka soko la kariakoo,ambapo lengo kubwa la maonyesho hayo ni kuzipa familia ambazo huwa zinatembelea fukwe hizo kufanya manunuzi yao kwa gharama nafuu kabisa
Wakina dada bidhaa zenu zinapatikana usikose

No comments: