Katika salamu zake, Malinzi amewapa pole familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki na wadau wa mpira wa miguu na kusema TFF ipo pamoja na wafiwa katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Wakati wa uhai wake marehemu Juma Ally Khamis alikuwa mwamuzi mwenye beji ya FIFA, mkufunzi wa waamuzi Tanzania, Meneja wa uwanja wa Amani – uliopo Zanzibar na mratibu wa michezo Wizara ya Habari na Utamaduni na Michezo kisiwani Zanzibar.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika leo Alhamis nyumbani kwake Pemba.
No comments:
Post a Comment