Benchi la ufundi lilimshauri Rais Malinzi kwamba kambi hiyo ipigwe jijini Victoria, kwenye Kisiwa cha Mahe nchini Shelisheli. Serengeti Boys inatarajiwa kuondoka nchini usiku wa kuamkia Jumatatu kwenda Shelisheli ambako itafanya mazoezi maalumu kwa ajili ya mchezo huo ambao utafanyika Septemba 18, 2016 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hii ni mara ya pili kwa Malinzi kutimiza ahadi yake kwa wachezaji hao. Kwa mara ya kwanza aliahidi kuwapa kambi ya nje kama wangewatoa Shelisheli. Timu kweli ilikwenda Madagascar kabla ya kuivaa Afrika Kusini ‘Amajimbos’ na kuitoa na kwa sasa inakwenda Shelisheli kujipanga kwa ajili ya kuitoa Congo-Brazzaville.
Serengeti Boys ambayo ilipiga kambi Hosteli za TFF, zilizo Karume kwa siku nne kabla ya safari hiyo na Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Bakari Shime maarufu kama Mchawi Mweusi amesema kwamba anaamini kuwa mchezo ujao utakuwa mgumu kwa kuwa kila timu itajipanga kuvuka ili kucheza fainali hizo.
No comments:
Post a Comment