Friday, November 18, 2016

KAMPUNI YA NISHATI JUA YAZINDUA KAMPENI YA “KUANGAZA AFRIKA”



Bi. Neela Krishnamurthy, Mkurugenzi mkuu wa Paraa Mwanga akizngumza na wanahabari Pamoja na wadauu mbalimbali wakati wa Uzinduzi huo wa kampeni maalum ya Kuangaza Africa iliyozinduliwa Leo Jijini Dar es salaam

Kampuni ya nishati ya jua ya jijini Dar es Salaam inayojulikana kama Paraa Mwanga Limited imezindua rasmi kampeni ya “Kuangaza Afrika.” Paraa Mwanga imezindua kampeni hiyo yenye lengo la kuleta mwanga katika nyumba za vijijini kupitia vifaa vya ubora wa juu vya nishati ya jua ikishirikiana na kampuni ya Indian Electronic na kampuni ya USA Electro mechanical.


Kampeni hiyo ambayo iko wazi kwa umma itawezesha familia nyingi kuweza kushinda vifaa vya ubora wa juu vinavyotumia nishati ya jua zikiwemo taa za mfumo wa LED, redio za FM, chaja za simu za mkononi na betri, vifaa vya kutengeneza umeme jua (solar panels), televisheni, ving’amuzi, majiko ya kutumia gesi na bima za afya ya jamii kila wiki. 

Bi. Neela Krishnamurthy, Mkurugenzi mkuu wa Paraa Mwanga akionyesha Baadhi ya Solar zao wanazosambaza ambazo zina Ubora wa aina yake
Shindano hili litafanyika kuanzia Novemba 2016 hadi Februari 2017 na linategemewa kufikia vijiji zaidi ya 6,000 katika kampeni hii itakayopita katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Lindi, Mbeya, Iringa, Mwanza na Arusha. Watakaovutiwa kushiriki wanashauriwa kujiandikisha kwa kutuma TZS 500, kwenda kwenye namba ya Airtel money 28668.

Bw. Said A. Shamo, Mwenyekiti wa Paraa Mwanga na Mwakilishi wa Baraza la Djibouti nchini Tanzania akizungumza wakati wa Uzinduzi huo Jijini Dar es salaam

Akizungumza katika mkutano na waandishi, Bi. Neela Krishnamurthy, Mkurugenzi mkuu wa Paraa Mwanga, alisema, “Tunajivunia kuweza kufanya promosheni ya vifaa vya LED na umeme jua katika vijiji vya Tanzania. Mahitaji ya nishati ya umeme ni makubwa kuliko uzalishaji na hivyo kupelekea asilimia kubwa ya vijiji kutokuwa na umeme. Bado kuna njia ndefu katika kufikia wale ambao hawafikiwi na mtambo wa nchi wa umeme. Ni lengo letu kuwa katika miaka miwili ParaaMwanga itaweza kuleta mwanga katika nyumba milioni moja nchini Tanzania.”

Bi. Krishnamurthy aliendelea kusisitiza kuwa katika mikoa mingi nchini shughuli za kibishara nyakati za usiku zinakuwa hazipo. Wanaume na wanawake wanashindwa kutumia muda wao kujiendeleza kiuchumi na watoto wanashindwa kujisomea wakati wa usiku. Vilevile, matumizi ya taa za mafuta ya taa na mishumaa ni gharama na sio salama kwa afya. “Nishati ya jua ndio suluhisho ya changamoto hizi na kupitia kampeni hii tutapatia nyumba, vijiji, shule na vituo vya afya vilivyopo vijijini fursa ya kuweza kupata vifaa bora kabisa vya nishati jua kutoka India ambavyo wanaweza kuvitumia katika maisha yao yote,” aliongeza Bi. Krishnamurthy.


Mteja wa kwanza kabisa Kutumia Bidhaa za Paraa Mwanga Bwana Colonel Mkami kutoka Jeshi la wokovu Tanzania akitia ushughuda Kuhusu ubora wa Bidhaa hizo leo Jijini Dar es salaam
Shindano hili ambalo limeshaanza litakuwa na droo za aina mbili kwa wiki, katika droo moja ya kawaida washindi kumi watazawadiwa vifaa vya nishati jua vya nyumbani vikiwemo, paneli za nishati jua (solar panels), betri na kidhibiti chake, taa za aina ya LED 3, redio ya FM na chaja ya simu. Kila wiki washindi kumi watazawadiwa ushindi wa draw hii.

Droo ya aina ya pili mshindi mmoja atapatiwa zawadi yenye taa za aina ya LED 4, redio ya sola inayotumia remote control na kifaa cha kusomea (flash reader), chaja ya simu na betri. Washindi hawa pia watapata televisheni ya inchi 24 ya aina ya LED, king’amuzi kilichounganishwa mwaka mmoja, jiko la gesi, feni na bima ya afya ya jamii. Kila wiki mshindi mmoja atajipatia zawadi ya draw ya pili.

Baadhi ya Solar zinazosambazwa na Para Mwanga na jinsi zinavyoweza kufanya kazi mbalimbali ikiwembo kuwasha Televission,Radio,Kucharge Simu,na huduma mbalimbali.
Pamoja na washindi wa wiki ambao watapatiwa vifaa vya nishati jua, pia makusanyo yatakayopatikana katika kampeni hii yatatumika katika kuweka mwanga katika vijiji vitakavyochaguliwa bure. 

“Kutokana na mafanikio yatakayopatikana katika kampeni hii, asilimia kadhaa ya makusanyo yatapelekwa katika vijiji katika mikoa ya Kigoma, Katavi, Kagera na Rukwa. Hii ni mikoa ambayo ina tatizo kubwa la kutokuwa na nishati ya umeme. Kwa kushiriki katika kampeni hii wote tutakuwa tunachangia katika kuleta mwanga na matumaini katika familia maeneo ya vijijini Tanzania,” alimalizia Bw. Said A. Shamo, Mwenyekiti wa Paraa Mwanga na Mwakilishi wa Baraza la Djibouti nchini Tanzania.

Wadau katika uzinduzi huo
Shindano liko wazi na washirki wote wanahimizwa kutuma TZS 500 kwenda kwenye namba ya Airtel money 28668.

No comments: