Friday, June 30, 2017

TAASISI YA LECRI CONSULT YAWAPA VIJANA ZAIDI YA 100, MBINU ZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO ZA AJIRA

Taasisi inayotoa huduma na ushauri wa kisheria na masuala ya haki za watoto na vijana ya  Lecri  Consult. Leo tarehe 30 ya mwezi juni imewakutanisha vijana zaidi ya 100 waliomaliza  vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kujitambua na kutambua fursa zilizopo mbele yao.
Mkurugenzi Mtendaji ambaye pia ni Mwanasheria wa Lecri Consult Bi. Edna Kamelek akiongea na wageni walioudhuria kwenye semina ya uwezeshaji vijana  iliyofanyika mapema leo jijini Dar es salaam

Akifungua semina hiyo mkurugenzi mtendaji wa Lecri Consult Bi. Edna Kamalek alisema kuwa semina hii imelenga kwa vijana waliomaliza vyuo ambao hawana ajira ili kuweza kuwajengea uwezo kutatua changamoto zao na kuwapa ujasiri pindi wanapohitajika kwenye usahili.

“Na kwa wale vijana waliopenda kujiajiri tunawajengea uwezo wa kujisimamia na kuendesha biashara zao binafsi” alisema mkurugenzi

Lakini pia kwa wale vijana ambao tayari wameshapata ajira wanapewa elimu, miiko na maadili ya kazi ili kuweza kuboresha ufanisi wao na wasifanye kazi kwa mazoea.
Naibu Mkurugenzi ofisi ya Waziri mkuu uamasishaji vijana na uwezeshaji vijana kiuchumi Bi. Esther Riwa kiongea na wageni waalikwa kwenye semina wa uwezeshaji vijana mapema leo jijini Dar es salaam
Akitoa elimu hiyo kwa vijana Naibu Mkurugenzi ofisi ya Waziri mkuu uamasishaji vijana na uwezeshaji vijana kiuchumi Bi. Esther Riwa alisema kuwa tatizo kubwa ni mitaala tuliyonayo  haimjengi mtoto akimaliza aje kupata ajira. “lakini pia tatizo lingine ni kutofuata maono vijana wengi huchagua masomo kwa kufuata mkumbo au kwa kushinikizwa na wazazi au walezi wao na mwisho wake kushindwa kufikia malengo waliyojiwekea ” alisema Bi Esther

Alisisitiza pia vijana wengi mitazamo yao ni kwamba wakimaliza kusoma moja kwa moja kuajiriwa na hivyo kushindwa kuzitafuta fursa za kujiajiri kwa kutumia rasilimali zilizopo hapa nchini kama kama ardhi kuwekeza kwenye kilimo, bahari, mali asili nk.


Bi. Estha alisema kuwa  vijana wengi wanapenda kuingia kwenye ujasiliamali  lakini hawana mbinu za kibiashara na matokeo yake ufanya biashara zenye kipato kidogo hali inayofanya kushindwa kufikia malengo yaliyowekwa na serikali ya kuondokana na umasikini. Na kwa kupitia semina vijana wataweza kuzinduka na kuziangalia fursa zenye matokeo mazuri hivyo kupunguza wimbi la umasikini kwa taifa.
baadhi ya wageni waalikwa walioudhuria kwenye semina ya uwezeshaji vijana iliyofanyika mapema leo jijini Dar es salaam
Bi. Estasia Ngowi akitoa mrejesho baada ya kupata nafasi  ya kuhudhuria tena kwenye semina ya uwezeshaji vijana iliyofanyika mapema leo jijini D
ar es salaam
Baadhi ya vijana walioudhuria semina hiyo

No comments: