Tuesday, August 29, 2017

KAMPUNI YA ITEL TANZANIA YAMWAGA VIFAA MBALIMBALI VYA MASOMO SHULE YA MSINGI UHURU ARUSHA

Meneja masoko Kanda ya kaskazini; Noel Mgasa akizngumza wakati wa utoaji vifaa vya masomo pamoja na bidhaa za mahitaji ya msingi kwa wanafunzi 76 wenye mahitaji maalum katika shule ya msingi Uhuru jijini Arusha.
 Kampuni ya simu za mkononi ya itel kwa kushirikiana na balozi wake Irene Uwoya, imetoa Msaada wa vifaa vya masomo pamoja na bidhaa za mahitaji ya msingi kwa wanafunzi 76 wenye mahitaji maalum katika shule ya msingi Uhuru jijini Arusha.

Afisa hABARI WA itel  Fernando Wolle Akizungumza katika hafla hiyo
Akikabidhi vifaa hivyo mwishoni mwa wiki balozi wa itel Irene Uwoya alisema jamii inapaswa kufahamu kuwa wapo wahitaji ambao wanataakiw kukumbukwa na jamii yao iliyowazunguka.
“Napenda kuwaasa Watanzania wenzangu kwamba kuna watu wanahitaji elimu lakini kuna vitu wanakosa vya kuwasaidia wapate hiyo elimu, suala la msingi ni kujitahidi mahali sahihi pa kupeleka msaada huo, sisi kama itel, tumeona ni vyema tuanze  kuleta hapa lshule ya Uhuru lakini tutaendeleza jitihada hizi kwasababu tunaamini elimu ndio kila kitu” Alisema Uwoya.
Balozi wa Itel Tanzania Msanii Irene Uwoya akimkabishi  Mwalimu mkuu  shule ya msingi Msingi Uhuru jijini Arusha.Zurina Rajabu msaada wa Vifaa mbalimbali
Naye  Meneja masoko wa kampuni ya itel  kanda ya Kaskazini Bwana Noel Mgasa alisema  wameamua kutoa msaada huo kutokana na shule hiyo kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wenye uhitaji.
“Kimsingi tumeamua kutoa msaada huu kwa kuona umuhimu wa jitihada zinazofanywa na walimu wa shule ya msingi Uhuru na wadau wengine wanaojali umuhimu wa elimu,na sisi tumeanzia Arusha lakini tutafika mpaka mikoa mingine” Alieleza Mgasa.

Kwa upande wake Afisa habari wa kampuni ya itel  Fernando Wolle alisema wametoa msaada huo kutokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya kampuni ya itel na jamii nzima ya Kitanzania.
“Hatuwezi tukajisifu kwamba ni sisi tuliotoa msaada huu, msaada huu unatokana na kuaminiana kati ya itel na Watanzania, kwa kifupi ni kwamba kama ulishawahi kununua simu ya itel basi wewe ndiye uliyewezesha, naomba tu Watanzania endeleeni kutumia simu zetu na kwa sasa tunayo itel S31, ukinunua basi unaunga mkono jitihada hizi” Alisema Wolle.
Akieleza kuhusu msaada huo Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Uhuru Zurina Rajabu alisema kampuni ya itel haijakosea kutoa msaada huo katika shule yake kutokana na uhitaji walionao.
“Tuna jumla ya wanafunzi wenye ulemavu wa akili 76, kwahiyo itel hamjakosea kabisa kuja hapa Uhuru kutoa msaada huu, hawa watoto ni binadamu kama walivyo wengine, na wengine tunawafundisha mpaka wanakuwa kawaida na wangine waliomaliza wana maisha mazuri tu kwahiyo tunaomba ushirikiano zaidi” Alisema Rajabu.


Shule ya msingi Uhuru ilianzishwa mwaka 1946 na mpaka sasa ina wanfunzi zaidi 1500 na kati yao wanafunzi 76 wana ulemavu wa akili.

PICHA ZOTE ZA HAFLA HIYO ZIPO HAPA---














No comments: