Monday, September 4, 2017

Jaji Mstaafu Thomas Mihayo Kuongoza Kamati ya Kutafuta Mzabuni Timu ya Simba

Jaji Mstaafu Thomas Mihayo Kuongoza Kamati ya Kutafuta Zabuni Timu ya Simba

Klabu ya Simba imemtangaza Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu, Thomas Mihayo kuwa  mwenyekiti wa kamati maalum ya  kumtafuta mzabuni ambaye atanunua hisa  asilimia 50  za timu hiyo  kwa mujibu wa mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Afisa Habari wa klabu hiyo, Hajji Manara imesema kuwa mbali ya Jaji Mstaafu huyo, wajumbe wengine wa kamati hiyo ni  Wakili Damas Ndumbaro, Mbunge wa Ilala, Azzan Zungu, mtaalam wa masuala ya manunuzi,  Yussuf  Majjid Nassor na Abdulrazak Badru ambaye ni Mkurugenzi wa Bodi ua Mikopo ya Elimu ya Juu Tanzania.

Manara alisema kuwa kamat hiyo itakutana  Septemba 7 (Alhamis) kuanza kazi ya kuwajadili wanachama ambao watataka kuzinunua hisa hizo ambapo watafuata sheria za manunuzi ya umma.

Sheria hiyo inawapa wanachama hao kukaa siku 45 kabla ya kumtangaza mzabuni wa timu hiyo kwa mujibu wa sheria. Klabu ya Simba imepyisha muunda mpya wa uendeshaji ambapo kwa sasa itakuwa chini ya utaratibu wa hisa.

Klabu hiyo itamiliki hisa 50 ambazo ni sawa na Sh bilioni 20  na asilimia zilizobaki zitakuwa kwa ajili ya wanachama au wabia ambao watagawana asilimia 50  (Sh bilioni 20).

“Nawaomba wanachama kuwa na utulivu mkubwa kwa kipindi hiki ambacho ni muhimu kuifanya klabu kuwa bora ndani na nje ya uwanja. Lengo ni kuwa katika mfumo wa kisasa ambao utaifanya klabu yetu kuwa bora Tanzania na nje ya mipaka yake,” alisema Manara.

No comments: