Friday, September 1, 2017

MAANDALIZI YA TAMASHA LA JINSIA YAPAMBA MOTO ANGALIA KITAKACHOJIRI KWENYE TAMASHA HILO

Ikiwa zimebaki siku chache kabla ya kufanyika kwa tamasha kubwa la jinsia linalotarajiwa kufanyika siku ya jumanne tarehe 5 mpaka 8 ya mwezi wa 9 katika viwanja vya mtandao wa jinsia TGNP.

Maandalizi yakiwa bado yanaendelea kwa upande wa wanaharakati wa semina za jinsia GDSS wameendelea kujipanga ipasavyo kuhakikisha wanaonyesha vitu vikubwa Zaidi kwa kuwa wao ndio wenyeji wa tamasha hili, na kusema kuwa hawatakubali kuja kufunikwa na wageni watakao kuja kwenye tamasha hilo.
Afisa Program na nguvu za pamoja wa TGNP Bi. Anna Sangai akiendesha semina ya GDSS kwa kuchukua maoni na kuangalia nini kifanyike kwenye Tamasha la Jinsia ili lizidi kuwa zuri zaid kwa mwaka huu.
Akiongoza semina hiyo afisa program wa nguvu ya pamoja Bi. Anna Sangai alisema maandalizi yanaendelea vizuri na kwa mwaka huu tamasha hilo litachukua Zaidi ya wanafunzi 150 wa shule za sekondari na msingi.

Miongoni mwa shule hizo ni shule ya msingi umoja na mabibo sekondari zilizopo kata ya mabibo kwa idadi ya 25 msingi na 25 sekondari ambazo zitakuja siku ya kwanza ambayo ni tarehe 5, na kundi la pili litakuwa kata ya mwananyamara ambalo pia ni wanafunzi 50, 25 shule ya msingi mchangani na shule ya sekondari makumbusho wanafunzi 25, na kundi la mwisho litakuwa shule ya msingi kilimani wanafuzni 25 na kipunguni sekondari wanafunzi 25 hizi toka kata ya kipunguni.

Aidha dada anna alipenda kuwasisitiza wanaGDSS kuwa wakarimu kwa wageni wote lakini pia kuwa na upendo ili wageni wajione wako nyumbani na kama ukiokota kitu cha mtu mwingine basi kipelekwe mahali husika ili kitangazwe na kupewa mwenye kitu chake ili wageni wafurahie tamasha na kuona TGNP ni sehemu nzuri na salama kwao.

Lakini sambamba na hilo wanaGDSS wametakiwa kuhakiki majina yao ili waweze kujua wamapangwa vitengo gani vya kutoa huduma na pia kwa ajiri ya kupewa vitendea kazi kama mabegi na Tshirt za tamasha hilo pamoja na huduma nyinginezo kama chakula nk.


Na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa makamu wa kwanza wa rais mwanamke kwa Tanzania mama samia suluhu hassani na kusema kuwa amashapelekewa barua hivyo wanatarajia kama hatokuwa na shughuli nyingi za kiserikali ataungana na jopo kubwa la wageni katika tamasha hilo.


baadhi ya washiriki wa semina ya GDSS ya wiki hii wakisikiliza kwa umakini muongozo unaotolewa na kiongozi wao.
Bi. Heriet Kabende akichangia mada katika semina ya jinsia na maendeleo GDSS ilifanyika jumatano hii ikiwa semina ya mwisho kabla ya siku ya tamasha la jinsia linalotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Bw. Innocent Siriwa akitoa maoni kuhusiana na Tamasha la Jinsia linalotarajiwa kuanzia jumanne ya tarehe 5 mpaka ijumaa 9 katika viwanja vya Mtandao wa Jinsia Mabibo jijini Dar es salaam

Bi. Subira Kibiga akiendelea kuwafua wanafunzi wake kwa upande wa mashairi ili waweze kutoa kitu kizuri siku ya Tamasha la Jinsia linarotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

No comments: