Friday, September 8, 2017

TGNP MTANDAO YAELEZA MIPANGO YAKE MIKUU MITATU BAADA YA TAMASHA LA JINSIA 2017

Wananchi  pamoja na waandishi wa habari waliopata nafasi ya kuhudhuria katika Tamasha la 14 la Jinsia mwaka 2017, wametakiwa kuwa na utamaduni wa kuhoji juu ya mipango na maazimio yanayowekwa baada ya kukamilika kwa tamasha hilo.
Mwenekiti wa bodi ya TGNP Mtandao Bi. Vicensia Shule akiongea na waandishi wa habari mapema jijini Dar es salaam
Akiongea na waandishi wa habari mapema leo mwenyekiti wa bodi ya TGNP Mtandao Bi. Vicensia Shule alisema kuwa leo tunahitimisha tamasha letu lililodumu kwa muda wa siku 4 kuanzia tarehe 5 mpka 8 ya mwezi septemba, hivyo basi wadau pamoja na waandishi wa habari muwe na utamduni wa kuwa mnatuhoji kuhusiana na kile tulichokipanga kama kweli tumeweza kukitimiza.

Miongoni mwa mipango hiyo ni kuhakikisha kuwa TGNP mtandao wanatafuta taarifa na kuzifanyia uchambuzi yakinifu ili kutoa takwimu sahihi kuhusu mimba na ndoa za utotoni, ukatili wa kijinsia na umiliki wa ardhi kwa wanawake na watu wenye ulemavu.

Na mpango wapili ni  kuendelea na utamaduni wake wa kutambua na kuenzi michango ya wanawake mbalimbali waliofanya vizuri katika kuleta maendeleo kwa ngazi jamii, taifa na kimataifa.
Lakini pia kutoa mafunzo ya kuchukua na kutunza kumbukumbu za wanawake hao na kuzisambaza kwa azaki, vijana na wadau mbalimbali ili waweze kujifunza kupitia wao lakini pia kuweza kurithi kati ya kizazi kimoja na kingine.

Bi vicensia aliendelea kwa kusema wataweka mipango endelevu ya kurithi ujuzi na maarifa kwa wanawake waliobobea katika tasnia mbalimbali kwa vizazi na lika moja kwenda lingine.

Alisema kuwa baadhi ya wanawake walioleta mabadiliko ya kweli na kuweza kutunukiwa tuzo ni kama Mheshimwa Samia Suluhu,Getrude Mongella,Spika mstaafu wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Anne Makinda,Profesa Daktari Esther Mwaikambo,Anna Abdallah na Esther Bulaya. 

Wengine ni wanachama wa TGNP Mtandao waliotoa mchango mkubwa katika kujenga Tapo la Ukombozi wa wanawake kimapinduzi akiwemo Profesa Marjorie Mbilinyi,Asseny Muro,Mary Rusimbi,Demere Kitunga,Subira Kibiga,Aggripina Mosha na Zippora Shekilango. 
Waandishi wa habari wakiendelea kuchukua matukio katika mkutano wa viongozi wa TGNP Mtandao na waandishi wa habari mapema jijini Dar es salaam.
Na bila kuwasahau vijana ambao ni zaidi ya asilimia 60 ya wananchi wa Tanzania  kuweza kushiriki katika Nyanja zote kuhakikisha rasilimali za kutosha zinatengwa kuhakikisha utekelezaji wa mipango na mikakati ya vijana inatekelezeka bila kuangalia itikadi, jinsi, dini, jografia na hali ya kimapato.



No comments: