Monday, October 30, 2017

KISHINDO CHA MSIMU WA TIGO FIESTA CHAACHA GUMZO MOSHI...

Wasanii Banarba na Gnako wakishiriki uzinduzi wa huduma mpya ya Tigo ya TUMEKUSOMA ambayo ni namba maalum (code number) itakayowawezesha wateja wa Tigo kuingia kwenye menyu na kupata huduma mbalimbali. Uzinduzi huo ulifanyika kwenye tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.

Msanii Bright akiwa kwenye jukwaa la Tigo Fiesta liliofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.

Chege akiburudisha kwenye jukwaa la Tigo Fiesta liliofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.

Msanii Bright akiwa kwenye jukwaa la Tigo Fiesta liliofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.

Umati wa wakazi wa Moshi wakiwa wanashuhudia burudani iliyokuwa inatolewa na wasanii .

Gigy Money akiwa katika jukwaa la Tigo Fiesta mapema usiku wa kuamkia jumatatu

Jux akiburudisha wakazi wa Moshi mapema usiku wa kuamkia jumatatu katika jukwaa la Tigo Fiesta .

TIGO Fiesta 2017 imefana vilivyo mkoani Kilimanjaro ambapo wasanii mbalimbali wa Bongo fleva wamefanya vilivyo katika viwanja vya Majengo katika Manispaa ya Moshi kwa kutoa burudani ya kukata na shoka kwa wakazi wa manispaa hiyo.
Katika kuhakikisha kuwa kila mkazi wa Moshi anafurahia vilivyo tamasha maalumu la Tigo Fiesta 2017 ambapo mdhamini mkuu wa tukio hilo la aina yake Tigo Tanzania leo wametangaza namba maalumu ya wateja ambayo ni *147*00# hii inajulikana kama TUMEKUSOMA ambayo  wateja wataweza kufanya kuitumia katika huduma mbalimbali za Tigo.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika tamasha maalumu la Tigo Fiesta 2017 katika Manispaa ya Moshi, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Tigo Tanzania, William Mpinga alifafanua kuwa, namba hiyo mpya (Code number) itatumika kwa wateja wa Tigo kote Tanzania katika kupata huduma mbalimbali za mtandao huo.

Tofauti na matukio  yaliyotangulia, washiriki wote kutoka mtandao wowote kwa tamasha la mwaka huu mbali na kupata huduma ya kulipia kiingilio kwa huduma ya Tigo-Pesa, pia wamepata burudani kabambe kutoka kwa wasanii mbalimbali wa muziki kutoka Tanzania.
Wasanii waliotumbuiza katika Tigo Fiesta katika viwanja vya Majengo katika Manispaa ya Moshi ni pamoja na Rich Mavoko, Chege, Nandy, Maua, Vanessa, Jux, Ben Pol, Rostam, Weusia, Darassa,Lulu Diva, Rosa Lee, Mimi Mars, OMG, Gigy Money,  Asley na wasanii wengineo.

Jukwaani Msanii Rosa Ree aliingia kama Malkia na kiti chake nakuwafanya mashabiki wapagawe na wimbo wake Mchagamchaga na nyingine,
Msanii Aslay kama ilivyokawaida yake mashabiki waliweza kuimba nae mwanzo mwisho wa nyimbo zake zote, wimbo wake mhudumu ndio uliwapagawisha zaidi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya kaskazini, Henry Kinabo amewataka watanzania kutumia huduma mbalimbali zitolewazo na Tigo kwa kuwa faida inayotokana na huduma inasasaidia huduma mbalimbali za kijamii zikiwemo elimu, afya na nyinginrezo ikiwamo mtandao wa intaneti.

“Nawashauri watanzania wote kutumia huduma mbalimbali bora zitolewazo na Tigo  kwani sehemu kubwa ya faida tunayopata tunairudisha kwa jamii kupitia huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo elimu hasa huduma ya intaneti kwashule mbalimbali, mbali madawati tuliyoto mwaka jana..” alifafanua Kinabo. 

No comments: