Thursday, February 1, 2018

TBL yashusha bei ya Castle Lite kutoka 2,500 hadi 2,000

Mkurugenzi wa Masoko wa TBL - Afrika Mashariki, Thomas Kemphuis akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo wakati akitolea ufafanuzi juu ya taarifa za kudukuliwa kwa mfumo wa mtandao wao wa kuhifadhi taarifa na kusisitiza kuwa mfumo wa taarifa zao zipo salama. Kushoto ni Meneja Masoko, Udhamini, Habari na Promosheni za Wateja - Afrika Mashariki, George Kavishe na Kulia ni Meneja Mawasiliano ya Nje wa TBL, Zena Tenga.


TBL yatoa ufafanuzi juu ya madai kudukuliwa mfumo wake wa taarifa

Yatangaza punguzo la bei ya rejareja kwa bia ya Castle Lite Premium Lager

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), leo imetoa ufafanuzi juu ya taarifa za kudukuliwa kwa mfumo wake wa kuhifadhi taarifa na kusisitiza kuwa mfumo wako na taarifa zake zipo salama.
Kwa siku kadhaa, kumekuwepo na taarifa kwenye vyombo mbali mbali vya habari kuwa, mfumo wa kuhifadhi taarifa wa TBL umedukuliwa na watu wasiojulikana na hivyo kuhatarisha kuvuja kwa taarifa zake muhimu.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Murugenzi wa Masoko wa TBL, (Afrika Mashariki), Thomas Kemphuis alisema, baada ya uchunguzi wa kina kampuni hiyo imejiridhisha pasipo na shaka kuwa hakuna tukio la aina hiyo lililotokea na kusisitiza taarifa zake zipo salama huku ikiwataka wanahisa wake, wadau pamoja na umma kwa ujumla kutokuwa na wasiwasi.

“Baada ya uchunguzi wa kina wa wataalamu wetu wa ndani na nje, TBL inapenda kuuthibitishia umma kuwa mfumo wetu wa kuhifadhi taarifa haujadukuliwa wala kuguswa kwa namna yoyote ile. Tunapenda kuwaambia wanahisa wetu, wadau na umma kwa ujumla wasiwe na wasiwasi kwa kuwa hakuna tukio la aina hii,” alisema Kemphuis.

 Akisisitiza nia ya TBL kuendelea kutoa huduma bora, Kemphuis alisema kampuni hiyo inachukulia kwa uzito mkubwa suala la usalama wa mifumo yake na ndiyo sababu ya kufanya uchunguzi wa haraka na wakina mara baada ya kupata taarifa za uvumi juu ya udukuzi.

“Usalama ni moja kati ya nguzo muhimu sana kwenye utendajii wa TBL. Tunafurahi kujivunia historia nzuri ya usalama ambayo tumekuwa nayo kwa miaka mingi,” alisema.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa TBL itaendelea kutengeneza mifumo imara ya ulinzi wa taarifa zake ili kuepuka matukio yasiyotarajiwa kama udukuzi.

Wakati huo huo, TBL imetangaza habari njema kwa wateja wake baada ya kutoa punguzo la bei kwa bia yake pendwa ya Castle Lite Premium Lager kutoka bei ya sasa ya shilingi elfu 2,500 hadi shilingi 2,000.

Kwa mujibu wa Kemphuis, punguzo hilo la bei ni zawadi kwa wateja wa bia hiyo kwa kuwa wateja waaminifu na zaidi kwa kuiunga mkono kampuni ya TBL kupitia bidhaa zake.

“Kupunguza bei ya bia ya Castle Lite Premium Lager kunadhihirisha shukrani zetu kwa wateja wetu kwa kutuunga mkono kwa kipindi kirefu. TBL siku zote ipo tayari kuwasikiliza wateja wake na kuwapa kile wanachokitaka,” alibainisha.

Kemphuis pia aliongeza kwamba wanaelewa kuhusiana na kushindwa kuleta tamasha hilo nchini ila akaeleza kuhusu utaratibu wa kuhakikisha Wanzania wanashiriki tamasha hilo.
“Tunajiandaa kuwapeleka watanzania 12 nchini Afrika ya kusini kuhudhuria tamasha la Castle Lite Unlocks litakalofanyika mwezi wan ne, utaratibu zaidi utatolewa,” alisema Kemphuis. 


No comments: