Friday, February 26, 2016
SDL KUMALIZIKA WIKIENDI HII
Kesho Ijumaa, michezo mitatu ya kundi C itachezwa katika raundi hiyo ya mwisho, Villa Squad watacheza dhidi ya Mshikamano (Mabatini, Mlandizi), Abajalo Dar v Karikaoo FC (Karume) na Changanyikeni watakuwa wenyeji wa Cosmopolitan katika uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha.
Kundi A, Jumamosi Green Warriors watawakaribisha Abajaro Tabora katika uwanja wa Mabatini Mlandizi, Transit Camp watakua wenyeji wa Mvuvumwa uwanja wa Kambarage Shinyanga, huku siku ya Alhamis Singida United watacheza dhidi ya Mirambo uwanja wa Namfua mjini Singida.
Jumamosi Kundi C, Alliance Schools watakua wneyeji wa Bulyankulu katika uwanja wa CCM Kirumba, JKT Rwamkoma watacheza dhidi ya Pamba FC uwanja wa Karume Musoma, na Madini FC watakua wenyeji wa AFC Arusha uwanja wa Mbulu.
Kundi D, Jumapili Mkamba Rangers watacheza dhidi ya Wenda FC uwanja wa CCM Mkamba, Sabasaba watakua wenyeji wa The Mighty Elephant uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, huku Mbeya Warriors wakicheza dhidi ya African Wanderes katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Timu moja ya kwanza kutoka katika kila kundi zitacheza hatua ya Fainali Machi 7-14, 2015 uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, ili kupata timu tatu za juu zitakazopanda moja kwa moja ligi daraja la kwanza (StarTimes League) msimu ujao.
Habari24 Blog yapaa kimataifa--HEINEKEN waonyesha kuguswa nayo
MAJALIWA AKUTANA NA MWAKILISHI WA UNHCR NCHINI
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi (UNHCR), Bi. Joyce Mends- Cole, Ofisini kwake jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
KAMPUNI YA MAWASILIANO YA TIGO YATOA MSAADA WA FEDHA ,KIASI CHA SHILINGI MIL TANO NA VIFAA VYA MICHEZO KWA WATOTO WA KITUO CHA AMANI CENTER CHA MJINI MOSHI.

Meneja wa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo kanda ya Kaskazini,Henry Kinabo (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 5 afisa uhusiano wa kituo cha kulea watoto waishio kwenye mazingira magumu cha Amani Center ,Kampuni ya Tigo imetoa kiasi hicho cha fedha pamoja na vifaa vya michezo kwa ajili ya maandalizi ya mbio za Kilimanjaro Marathoni.
Meneja wa kampuni ya Tigo Kanda ya Kaskazini,Henry Kinabo akikabidhi fulana kwa watoto waishio katika mazingira magumu ya Kituo cha Aman Center cha mjini Moshi.
Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini ,Henry Kinabo akifurahia jambo na afisa uhusiano wa kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu cha Amani Center ,Salma Khatibu,wengine ni watoto waishio katika kituo hicho.
………………………………………………………………………………………………………..
Wednesday, February 24, 2016
CUF Watoa Tamko Zito Kuhusiana Na Kukamatwa Kwa Mwanamkakati wa Maalim Seif
Wiki
iliopita, mnamo tarehe 16 Februari, 2016, aliyekuwa mjumbe wa Timu ya
Kampeni ya Chama Cha Wananchi (CUF), Ndugu Mohamed Ahmed Sultan
Al-Mugheiry (maarufu kwa jina la Eddy Riyami), alipokea barua ya wito
kutoka kwa Jeshi la Polisi Zanzibar ikimtaka kufika Makao Makuu ya
Polisi, Ziwani, Zanzibar siku inayofuata, yaani tarehe 17 Februari,
2016, saa 2 asubuhi kwa kile kilichoelezwa kwamba “kuna mambo muhimu
yanayomhusu” ambayo walitaka kuzungumza naye.
Mgambo wasio waadilifu kushughulikiwa
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Kutokana na tabia ya baadhi ya
mgambo katika Halmashauri za Jijini la Dar es Salaam kujipatia fedha kwa
njia zisizo za halali, serikali kupitia Halmashauri zake imejipanga
kuwachukulia hatua za kisheria migambo wote watakaobainika
kujishirikisha na vitendo vya rushwa.
Akitoa ufafanuzi juu ya madai ya
wanachi juu ya mgambo wanaochukua rushwa nje ya faini halali
zinazistahili kutozwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Wilaya ya Ilala,
Afisa Habari wa Manispaa ya Ilala Tabu Shabibu amesema kuwa zipo baadhi
ya taarifa wamepewa na watawachukulia hatua kwa kuwasitishia mikataba
wale wote watakaobainika kukiuka sheria na taratibu za kazi.
Tuesday, February 23, 2016
WAKULIMA WILAYANI RORYA MKOANI MARA WAPATIWA MAFUNZO YA KUPATA HUDUMA ZA UGANI KWA NJIA YA SIMU
Mtafiti Kiongozi Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (katikati), akizungumza na wakulima wa Wilaya ya Rorya Mkoani Mara katika mafunzo ya siku moja kwa wakulima hao ya kutumia simu kupashana habari za kilimo na kujua changamoto zinazo wakabili. Kulia ni Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia za Kilimo Afrika (OFAB), Daniel Otunge na kushoto ni Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Emmarold Mneney.
Maofisa Ugani wa Wilaya ya Rorya wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Rorya, Dominick Ndentabura akizungumza na wakulima hao kabla ya kuanza kwa semina hiyo.
Mkulima Sophia Charles kutoka Kijiji cha Roche akizungumzia changamoto ya ukosefu wa soko la zao la mhogo ambapo wanategemea zaidi soko nchini Kenya.
Mkulima Charles Ruola akizungumzia changamoto ya kilimo cha mahindi.
TFF, KTA ZAZINDUA PROGRAMU YA MAENDELEO YA SOKA KWA WANAWAKE
Monday, February 22, 2016
Meya wa kinondoni na DC MAKONDA kuna kitu kinaendelea,Soma kauli ya meya huyo hapa

Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob amemuonya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda kuacha tabia ya kuingilia majukumu ya Halmashauri, badala yake afanye kazi zinazomuhusu.
KATIBU MKUU BAWACHA AZINDUA RASMI OFISI MPYA YA MBUNGE WA VITI MAALUMU MKOANI MWANZA.
Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake
Chadema Taifa BAWACHA na Mbunge Viti Maalumu Taifa Grace Tendega (katikati) jana February 20,2016 akizindua ofisi Mpya ya Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza Chadema, Susan Masele (Kulia). Kushoto ni Paschazia Renatus ambae ni Katibu wa Bawacha Mkoa wa Mwanza.
Chadema Taifa BAWACHA na Mbunge Viti Maalumu Taifa Grace Tendega (katikati) jana February 20,2016 akizindua ofisi Mpya ya Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza Chadema, Susan Masele (Kulia). Kushoto ni Paschazia Renatus ambae ni Katibu wa Bawacha Mkoa wa Mwanza.
Akizungumza katika Uzinduzi huo, Tendega alipongeza uwepo wa ofisi hiyo ambayo itakuwa ikisikiliza kero za wananchi bila kujalisha itikadi zao za kisiasa kwa ajili ya kupokea hoja za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi ikiwemo kuzisemea bungeni.
“…Kazi ya Mbunge siyo kugawa hela. Kazi ya Mbunge ni kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua. Na mimi niseme nitakuwa mwakilishi bora na hapa tumeanza tu ambapo katika ofisi hii nitakuwa napokea na kusikiliza kero za wananchi na kwenda kuzisemea bungeni… Alisema Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza Chadema, Susan Masele.
Ofisi hiyo inapatikana Mtaa wa Ghana Green View, Kata ya Nyamanoro, Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza. Ndani yake pia kuna Ofisi ya BAWACHA Mkoa wa Mwanza.
Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema Taifa BAWACHA na Mbunge Viti Maalumu Taifa Grace Tendega (katikati) jana February 20,2016 akizindua ofisi Mpya ya Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza Chadema, Susan Masele. Kushoto ni Paschazia Renatus ambae ni Katibu wa Bawacha Mkoa wa Mwanza.
Kulia ni Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema Taifa BAWACHA na Mbunge Viti Maalumu Taifa Grace Tendega akiwa pamoja na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza Chadema, Susan Masele
Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema Taifa BAWACHA na Mbunge Viti Maalumu Taifa Grace Tendega akizungumza katika uzinduzi wa ofisi ya Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza (Chadema).
DK SHEIN AZUNGUMZA NA UVCCM MKOA WA MJINI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Mkoa wa Mjini kichama leo katika ukumbi wa CCM Amani Mjini Unguja na kuwataka Vijana kulinda Muungano na Mapinduzi ya Zanzibar,ikiwa ni katika hatua za uimarishaji wa Chama cha Mapinduzi,[Picha na Ikulu.]
KIKWETE AZINDUA OFISI YA CCM WILAYA YA KIBAHA MJINI LEO
Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akizindua Ofisi ya CCM Wilaya ya Kibaha mjini mkoani Pwani leo. Ofisi hiyo imejengwa na familia ya Mbunge wa Kibaha mjini Slyvester Koka (kulia). (Picha na Bashir Nkoromo).
Subscribe to:
Posts (Atom)







