Tuesday, July 12, 2022

BEI YA UMEME KUTOKA MIRADI MIDOGO YA UMEME SASA NI SHILINGI 1600

 

Waziri wa Nishati, January Makamba akizungumza na Bw.Muhonja Antony ambaye anafanya kazi za uchomeleaji katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Waziri wa Nishati alifika kisiwani humo ili kukagua hali ya upatikanaji umeme unaozalishwa kwa kutumia mitambo ya umeme Jua.

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akitazama nguzo za umeme zilizobeba nyaya ambazo zimesimikwa chini ya ziwa Victoria ili kupeleka umeme kwenye kisiwa cha Ukerewe kutokea Bunda –Mara.

Nguzo za umeme zilizobeba nyaya ambazo zimesimikwa chini ya ziwa Victoria ili kupeleka umeme wa kiasi cha megawati 10 kwenye kisiwa cha Ukerewe kutokea Bunda –Mara.

Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba (kulia) akizungumza na mwananchi katika Kijiji cha Kibara wilayani Bunda baada ya kuona jinsi vituo vidogo vya mafuta vijijini vinavyofanya kazi na kuwaeleza wananchi kuhusu fedha zilizotengwa na Serikali takriban shilingi Bilioni 10 ili kuwakopesha wananchi wanaotaka kuwekeza kwenye vituo vidogo vya mafuta vijijini.

Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba akizungumza na wanachi katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe wakati alipofika kisiwani humo kutatua changamoto ya upatikanaji wa umeme pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

…………………

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba, amesema kuwa, shilingi 1600 itakuwa bei mpya ya umeme kwa unit katika miradi midogo ya umeme iliyo nje ya Gridi ambayo itaanza kutumika tarehe 1 Agosti, 2022 ili kufanya wananchi kupata umeme wa uhakika na wawekezaji binafsi kuweza kujiendesha na kuwekeza zaidi.

Makamba amesema hayo tarehe 12 Julai 2022 akiwa katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza wakati alipofika kisiwani humo kutatua changamoto ya muda mrefu ya upatikanaji umeme wa uhakika.

Maamuzi hayo ya Serikali yamekuja baada ya wawekezaji binafsi wa miradi midogo ya umeme kutakiwa kuuza bei ya umeme kwa Shilingi 100 kwa unit gharama ambayo iliwapa changamoto za kiuendeshaji na hivyo kushindwa kuwapa wananchi huduma ya umeme ya uhakika.

Akiwa kisiwani Ukara, Makamba alielezwa na wananchi wa kisiwa hicho kuwa, awali walikuwa wakilipa Shilingi 3500 kwa unit na walikuwa wakipata umeme kwa masaa 24 kwa siku lakini baada ya kutangazwa kwa bei ya umeme ya shilingi 100, kampuni ya JUMEME inayotoa huduma ya umeme kisiwani humo ilianza kuwapa umeme kwa masaa Sita tu kwa siku na pia kutakiwa kununua umeme kwa tokeni.

Akitoa ufafanuzi kwa wananchi kuhusu upangaji wa bei za nishati, alieleza kuwa unapaswa kuhusisha pande zote mbili ambazo ni Mwekezaji na Serikali hivyo, zoezi la upatikanaji wa bei mpya ya umeme limekuwa la uwazi na kwamba gharama mpya iliyotajwa haipo juu kama awali ili kutowaumiza wananchi na pia haitakuwa Shilingi 100 ili kampuni binafsi nazo ziwe na uwezo kufanya shughuli zake kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Ameeleza kuwa Sera ya Nishati imetamka wazi kuhusu bei ya nishati inayopangwa na Serikali ikiwemo umeme, gesi na mafuta, kuwa lazima iendane na gharama za kuzalisha nishati husika.

Pamoja na kutangaza bei hiyo mpya, Waziri wa Nishati amezitaka kampuni husika kuhakikisha kuwa wanatoa umeme wa uhakika, wawasilishe mpango wa Biashara serikalini pamoja na kuwa na mkataba wa huduma kwa mteja.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya JUMEME, Bi. Aida Kiangi aliahidi mbele ya wananchi wa UKARA kuwa kuanzia tarehe 1 Agosti, 2022 umeme kisiwani humo utatolewa kwa masaa 24.

Katika hatua nyingine, Waziri Makamba ameendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kugawa mitungi ya gesi 167 ambayo itasambazwa kwa Shule za Serikali za Msingi na Sekondari kisiwani Ukara pamoja na walimu wa shule hizo ili wawahamasishe wananchi wengine kutumia nishati safi.

Awali, Waziri wa Nishati alikagua vituo vidogo vya mafuta wilayani Bunda, Mkoa wa Mara katika Kijiji cha Guta B na Kibara ikiwa ni mkakati wake wa kupeleka vituo vya mafuta hadi vijijini ili wananchi wapate Nishati safi na katika mazingira salama ambapo katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi Bilioni 2 ili kutoa mikopo kwa wananchi wanaotaka kuwekeza katika ujenzi wa vituo hivyo vijijini.

Akiwa safarini kuelekea wilayani Ukerewe Waziri Makamba alikagua nyaya za umeme zinazopita chini ya Ziwa Victoria ambazo zinapeleka umeme wa kiasi cha megawati 10 wilayani humo zikitokea Kisorya wilayani Bunda.

WAZIRI MKENDA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI JENGO LA MAKTBA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amezindua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la Maktaba la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kivukoni Jijini Dar es Salaam, mradi ambao utagharimu zaidi ya Shilingi bilioni 14 ili kuboresha mazingira ya Kufundishia na kujifunzia.

Jiwe la Msingi lililowekwa na Waziri Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof, Adolf Mkenda mapema leo Mkoani Dar es salaam. 

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo Profesa Mkenda alisema mpango wa sasa wa Serikali katika Sekta ya Elimu ni kuzalisha wasomi watakaokuwa na Elimu ya Kujitegemea kwa kuboresha mitaala ambayo mpaka sasa zaidi ya wadau laki moja wamekwisha toa maoni yao.

Prof. Mkenda amesema ubora wa Elimu ni ajenda ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambayo inahitaji mageuzi ili kuongeza ubora na iakisi mahitaji ya nchi, utandawazi kwa lengo la kuongeza uwekezaji.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Francis Maiko amekipongeza Chuo hicho kwa kutenga bajeti kiasi cha asilimia arobaini ambazo ni  fedha za ndani kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo.

“Hiki kilichofanywa na Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kinatakiwa kiwe mfano wa kuigwa na Taasisi nyingine ili kuwezesha Serikali kuendelea kutumia bajeti zinazotengwa kwa lengo la kuboresha zaidi Miundombinu ya Kufundishia na kujifunzia,”alisisitiza Prof Mkenda.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Shadrack Mwakalila amesema ujenzi wa jengo hilo utakuwa na Maktaba, Ukumbi wa Mihadhara pamoja na ofisi za wafanyakazi.

“Tumekusanyika leo hapa kwa ajili ya hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa jengo la Maktaba lenye uwezo kuchukua wanafunzi 2500, Ukumbi wa Mihadhara wa kutosha Wanafunzi 1000 pamoja na ofisi za Wafanyakazi,”alisema Prof. Mwakalila.

Aidha Mchakato wa Mradi huo waa Maendeleo ulianza katika bajeti yam waka 2018/2019, hata hivyo pamoja na kutengewa bajeti ya Maendeleo lakini fedha za miradi ya Maendeleo hazikutolewa hivyo katika bajeti yam waka 2021 Chuo kiliamua kutenga bajeti ya asilimia 40 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Prof. Mwakalila aliitaja miradi mimngine inayosimamiwa na Chuo hicho kuwa ni mradi wa ujenzi wa jengo la hosteli ya Wanafunzi katika Kampasi ya karume Zanzibar lenye uwezo wa kulaza Wanafunzi 1536 ulioanza Julai 18, 2021 na utagharimu zaidi ya bilioni 15.

Msimamizi wa mradi huo kutoka Wizara ya Ujenzi  Mhandisi Mwesigwa Ichwekeleza alisema mpaka sasa ujenzi umefikia asilimia 5 na utakuwa ni wa ghorofa 3 ambao utakamilika ndani muda wa miezi 30 kama ilivyopangwa.

                                                               Habari Picha..

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akiongea na Wanafunzi Pamoja na Wageni mbalimbali waliyofika kushuhudia Zoezi la Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Maktaba na Kumbi za Midahalo katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere leo Mkoani Dar es salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dkt. Francis Maiko Akiongea mbele ya Wageni mbalimbali waliyofika kushuhudia Zoezi la Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Maktaba na Kumbi za Midahalo katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere leo Mkoani Dar es salaam.
Waziri Mstaafu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mh. Stephen Wasira akiongea na Wageni katika tafrija ya uwekaji jiwe la Msingi Chuoni hapo, mapema leo Mkoani Dar es slaam.
Mkuu wa Chou cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Shadrack Makalila, akiongea na Wanafunzi Pamoja na Wageni mbalimbali waliyofika kushuhudia zoezi la Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Maktaba na Kumbi za Midahalo katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mapema leo Mkoani Dar es salaam.
Meza kuu ikipatiwa maelezo ya picha na Mkandarasi namna jengo litakavyokuwa baada ya kukamilika.
Zoezi la Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Maktaba na Kumbi za Midahalo katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere likiendelea leo Mkoani Dar es salaam.
Baadhi ya Washiriki wakifuatilia matukio katika zoezi la Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Maktaba na Kumbi za Midahalo katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere leo Mkoani Dar es salaam.


Monday, July 11, 2022

Prof. MKENDA: WAOMBAJI MIKOPO 2022-2023 SOMENI MWONGOZO.

 Waziri wa ElLmu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji Mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi HESLB, Prof. Hamisi Dihenga. Hafla hiyo imefanyika leo Jumanne Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.

Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta (TPC), Macrice Mbodo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) Angela Anatory akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Abdul-Razaq Badru akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Prof. Hamisi Dihenga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar (ZHELB) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. James Mdoe akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Uombaji Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 12, 2022 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA NA HESLB)

******************************

Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amewahimiza waombaji mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka 2022/2023 kusoma na kuuzingatia ‘Mwongozo wa Utoaji Mikopo kwa 2022/2023’ ili kuwasilisha maombi kwa usahihi.

Prof. Mkenda ameyasema hayo katika hafla fupi ya kuzindua mwongozo huo iliyofanyika katika ofisi za HESLB jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa HESLB Prof. Hamisi Dihenga na wadau wengine wa HESLB.

Prof. Mkenda amesema: “Kuanzia leo (Jumanne, Julai 12), mwongozo huu utapatikana katika tovuti ya HESLB (www.heslb.go.tz) na ya Wizara (www.moe.go.tz) katika lugha mbili za Kiswahili na Kiingereza … na kuwapa fursa waombaji kuusoma.  Dirisha la kupokea maombi ya mikopo kwa njia ya mtandao linatarajiwa kufunguliwa Julai 19 hadi Septemba 30, 2022,” amesema na kuongeza:

“Dirisha la maombi ya mikopo kwa mwaka wa masomo 2022/2023 litakuwa wazi kwa muda wa siku 70 kuanzia Julai 19 hadi Septemba 30 mwaka huu, hivyo tunawasihi wanafunzi waombaji wasome mwongozo kabla ya kuomba mkopo kwa kuwa ndiyo unataja sifa, vigezo na utaratibu wa kuomba mkopo,” amesema Prof. Mkenda.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. James Mdoe amewakumbusha waombaji mikopo kuzingatia maelekezo yaliyomo kwenye mwongozo ili kuondokana na changamoto ambazo hujitokeza kwa waombaji.

“Uzoefu unaonesha kuwa wanafunzi waombaji wamekuwa hawazingatii taratibu wakati wa kufanya maombi. Tunawasii mzingatie maelekezo ya mwongozo. Wakati wa dirisha la maombi kumekuwepo na changamoto nyingi zinazojitokeza kwa waombaji”, amesema Prof. Mdoe.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema kila mwaka mwezi Julai, HESLB huanza kupokea maombi ya mkopo kwa mwaka wa masomo unaofuata ambapo mwongozo huo hutoa maelezo ya kina kuhusu sifa na utaratibu wa kupanga mikopo kwa mwaka husika.

“Mwongozo huo umekamilika na kuidhinishwa na Bodi ya Wakurugenzi. Kuanzia wiki ijayo, tutaanza kuendesha programu za elimu kwa umma kupitia redio, televisheni, mikutano katika Kambi za JKT na mitandao ya kijamii” amesema Badru.

Katika mwaka wa masomo 2022/2023, Serikali imetenga kiasi cha TZS 573 bilioni kwa ajili ya kutoa mikopo na skolashipu kwa wanafunzi wa elimu ya juu nchini.

Tuesday, July 5, 2022

Luiza Mbutu "Tunaisuka CHAMUDATA Mpya wasanii wa Dansi nchi nzima waje kujiunga".

Na Muandishi wetu.

Chama Cha Muziki wa Dansi Nchini (CHAMUDATA) kimewataka wasanii wote wa Muziki wa Dansi kujitokeza kuhisajili kwenye chama hicho pamoja na Baraza la Sanaa la Taifa( BASATA) ili kuwawezesha kutambulika.
Mwenyekiti wa CHAMUDATA Luizer Nyoni(Luiza Mbutu) akiongea na waandishi wa Habari ambao hawapo pichani mapema leo mkoani Dar es salaam.
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Luizer Nyoni maarufu Kama mama "Luizer Mbutu"wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari kuelezea mwelekeo mpya wa Chama hicho baada ya kupata uongozi mpya 

Amesema kwamba wasanii wengi wa Dansi hawajajisajili kwenye Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na CHAMUDATA hivyo kutokana na kupatikana na uongozi mpya wa Chama hicho kinawasihi kuhisajili ili kufikia malengo yao kwani CHAMUDATA ya Sasa imejiwekea malengo makubwa.

"Sisi kama viongozi wapya tuna  vipaumbele kumi tutakavyo vitekeleza ikiwa ni pamoja na kueneza CHAMUDATA nchi nzima, kuandaa semina ya mafunzo ya hakimiliki na hakishiriki na mirahaba ambapo tayari tumezungumza na COSOTA ili watupe mafunzo,pia kukutana na viongozi wa bendi mbalimbali ili kuainisha changamoto zinazowakabili Wanamuziki na Biashara ya Muziki Kwa Ujumla." amesema Luizer

Nakuongeza kuwa vipaumbele vingine ni kushirikiana na vyombo vya habari katika kuutangaza Muziki wa Dansi,kutengeneza tovuti ya CHAMUDATA Ili kusaidia wanachama kuhisajili kidigitali,kusimamia masuala ya Bima ya afya Kwa wanachama,kuiwezesha CHAMUDATA kuwa karibu na serikali ili kutatua changamoto zinazowakabili,kuhakikisha bendi zote zinazofanywa maonyesho zimesajiliwa BASATA pamoja na kuandaa Tamasha kubwa la Muziki wa Dansi.
Katibu Mkuu wa CHAMUDATA Bw. Said Kibiriti akijibu swali la Muandishi wa habari mapema leo Mkoani Dar es salaam.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CHAMUDATA  Bw.Said Kibiriti amesema kwamba uongozi uliopo Kwa sasa ni uongozi mpya,baada ya kukabidhiwa ofisi na uongozi wa zamani baadhi ya nyaraka za ofisi hazipo nakwamba baada takufatilia wamebaini baadhi ya viongozi hao wameshafariki,hivyo kumekuwepo na madeni huku akaunti za chama  za  NMB na CRDB zikiwa hazina fedha.

" Hatuna Hesabu Sahihi ya madeni kwasasa,lakini bado tunaendelea kuyakusanya na yakiwa tayari tutawafahamisha wanachama,kwasasa tuanaendelea kukiimarisha chama kwani kimeanzishwa tangu mwaka 1986 lakini bado kimekuwa hakifahiki vizuri kwa wanamuziki wa Dansi Nchi nzima" amesema Bw.Kibiriti.
Mkutano ukiendelea.

Monday, July 4, 2022

MHE. MCHENGERWA SERIKALI KUJENGA STUDIO KILA WILAYA NCHINI

Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema Serikali inakwenda  kutengeneza studio kila wilaya kwa ajili ya kurekodia kazi za sanaa.
Mhe. Mchengerwa ameyasema haya leo Julai 3, 2022 wakati akifunga tamasha la kwanza la  kitaifa la utamaduni katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Amesema wizara yake inakwenda  kutekeleza maelekezo ya viongozi wetu ya kuthamini, kuandaa  mavazi ya taifa ili kuhakikisha mila na desturi za mtanzania zinaendelezwa.

"Maelekezo ya viongozi wetu ni sheria, amri iwe jua, iwe mvua  sisi Wizara, tutawajibika kutekeleza bila kusita wala kuchelewa" Amesisita Mhe. Mchengerwa

Pia amesema  wizara imejipanga vizuri kuhakikisha Tamasha la kitaifa la pili la Utamaduni litakalofanyika mwakani litakuwa katika kiwango cha kimataifa.

Ameongeza kuwa kumalizika  kwa tamasha hili ni mwanzo wa kuanza maandalizi ya matamasha kwenye mikoa  na wilaya zote nchini ambapo ametaka maafisa utamaduni kulisimamia hili.

"Ni matarajio yangu kuwa mikoa yote itakaoanza sisi kama wizara tutakuja mara moja. Tunahitaji watanzania wakae katika furaha katika maisha yao" amefafanua Mhe. Mchengerwa

Amewapongeza wakuu wa mikoa  kwa kuwezesha  vikundi  vya Utamaduni kuhudhuria kwenye tamasha.

Amesema  bila Utamaduni taifa hili litaendelea kukopa tamaduni za mataifa mengine.

Aidha, amesema  kufanikiwa kwa tamasha hili kuonekana  ni kutokana na maono ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan 

Amesisitiza kuwa tamasha hili litakuwa endelevu na litakuwa  linafanyika kwa mzunguko kila mkoa.

Pia amesema Wizara imefanikiwa kulitangaza tukio hili kwa  kuwa watu zaidi ya milioni  10 wametazama kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.

"Niseme kwa hili tumefanikiwa" amepongeza Mhe. Mchengerwa

Kwa upande mwingine Selikali imeanzisha Mfuko wa Utamaduni kwa lengo la kuwasaidi wasanii nchini ambapo amesema tayari kwa mwaka 2022/2023 umetengewa shilingi bilioni mbili kwa kazi hiyo.

Amewaomba viongozi wa mila  na wananchi kwa ujumla kuendelea kukemea vitendo ambavyo ni kinyume cha maadili ya mtanzania.

Pia amewataka wananchi kushiriki kwenye sensa.

Katika tamasha  hilo amekadhi zawadi kwa washindi wa ngoma na vyakula ambapo washindi wa ngoma za asili ni mkoa wa
Mwanza ambao umekuwa namba moja, Lindi ambao umekuwa namba mbili na mkoa wa
Mjini magharibi umekuwa wa tatu.

Kwa upande wa vyakula vya asili mkoa Kilimanjaro umeongoza ukifuatiwa na mkoa wa Tanga na mkoa wa Kagera umeshika nafasi ya tatu

   Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa akikabidhi Zawadi kwa  Vikundi vya Ngoma za Asili vilivyofanya vizuri vikiongozwa na Mkoa wa Mwanza, wakifuatiwa na Lindi na mshindi wa tatu ni Mkoa wa Magharibu kutoka Zanzibar katika  kucheza ngoma za Asili kwenye  Tamasha la kwanza la Kitaifa la Utamaduni lililofanyika Julai 01 hadi 03,Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Sunday, July 3, 2022

Makinda atinga kwenye Mnada wa Old Shinyanga Akihamasisha Wananchi kushiriki Sensa

 





Makinda ametembelea katika Mnada huo leo Julai 3,2022 akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na wananchi kwenye mnada huo, amewasihi siku hiyo ya zoezi la kuhesabiwa Sensa ya Watu na Makazi Agosti 23 mwaka huu, washiriki kikamilifu , ili Serikali ipate idadi ya watu wake kamili kwa kila eneo kuanzia ngazi ya chini.

“Tunaendesha zoezi la Sensa ya watu na makazi ili tujue Tanzania tuko watu wangapi, na itaisaidia Serikali katika upangaji wa mipango ya maendeleo kwa wananchi wote kulingana na idadi yao,” amesema Makinda.

“Rais Samia Suluhu Hassani amekuwa akitafuta fedha za maendeleo kwa wananachi wake, na anataka kujua ni maeneo gani ambayo wananchi bado hawana maendeleo kwa uwiano sawa na idadi yao, hivyo nawasihi jitokezeni kuhesabiwa Sensa,” ameongeza.

Aidha, amewataka pia wananchi watoe ushirikiano kwa Makarani wakati wa Sensa pamoja na kutoa taarifa za kweli na usahihi na siyo kudanganya ili siku huduma zikianza kutolewa na Serikali katika eneo husika kusiwepo na mapungufu.

“Kama wewe una ng’ombe 100 wataje wote usiseme una ng’ombe 10, ili siku madawa yakija kulingana na idadi ya mifugo mlioitaja msianze kugombania na kulalamika madawa hayatoshi na wakati awali nyie ndiyo mlitoa taarifa siyo sahihi,” amesema Makinda.

Katika hatua nyingine, amewataka wananchi wasiwafiche ndani watu wenye ulemavu pamoja na wazee, bali wawape fursa nao ya kuhesabiwa katika zoezi hilo la Sensa.

Nao baadhi ya wananchi waliokuwa kwenye mnada huo pamoja na wafanyabiashara, wameshukuru kupatiwa elimu hiyo kuhusu Sensa ya Watu na Makazi.

Kamisaa wa Sensa ya watu na Makazi Mhe. Anne Makinda akizungumza katika Mnada wa Old Shinyanga na kutoa elimu ya Sensa ya watu na makazi kwa wananchi na kuwahamasisha washiriki kikamilifu kuhesabiwa katika zoezi hilo la Sensa Agosti 23 mwaka huu.

Kamisaa wa Sensa ya watu na Makazi Anne Makinda akizungumza katika Mnada wa Old Shinyanga na kutoa elimu ya Sensa kwa wananchi na kuwahamasisha washiriki kikamilifu kuhesabiwa katika zoezi hilo la Sensa Agost 23 mwaka huu.

Mtakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu NBS Pastory Ulimali akizungumza kwenye Mnada huo wa Old Shinyanga.

Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akizungumza na wananchi kwenye Mnada huo wa Old Shinyanga wakati wa utolewaji wa elimu ya Sensa.

Wananchi wakisikiliza elimu ya Sensa na kuhamasishwa washiriki kuhesabiwa Agosti 23 mwaka huu.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya Sensa.

Elimu ya Sensa ikiendelea.

Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi Mhe. Anne Makinda akiwa katika Mnada wa Olshinyanga kutoa elimu ya Sensa na kuhamasisha wananchi washiriki kikamilifu kuhesabiwa Sensa Agosti 23 mwaka huu.

Kamisaa wa Sensa ya watu na Makazi Anne Makinda akiwa katika Mnada wa Old Shinyanga kutoa elimu ya Sensa na kuhamasisha wananchi washiriki kikamilifu kuhesabiwa Sensa Agosti 23 mwaka huu.

Kamisaa wa Sensa ya watu na Makazi Mhe. Anne Makinda akiwa katika Mnada wa Old Shinyanga kutoa elimu ya Sensa na kuhamasisha wananchi washiriki kikamilifu kuhesabiwa Sensa Agosti 23 mwaka huu.


Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi  Mhe. Anne Makinda akiwasili katika Mnada wa Old  Shinyanga kutoa elimu ya kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa  ya watu na makazi Agosti 23 mwaka huu.

Kamisaa wa Sensa ya watu na Makazi Anne Makinda akiwa katika Mnada wa Old Shinyanga kutoa elimu ya Sensa na kuhamasisha wananchi washiriki kikamilifu kuhesabiwa Sensa Agosti 23 mwaka huu.
Kamisaa wa Sensa ya watu na Makazi Anne Makinda akiwa katika Mnada wa Old Shinyanga kutoa elimu ya Sensa na kuhamasisha wananchi washiriki kikamilifu kuhesabiwa Sensa Agost 23 mwaka huu.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

IGP Siro apongezwa kwa kuleta maendeleo katika Kanisa

 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (kushoto) akipokea Baraka kutoka kwa Mhashamu Baba askofu Simon Masondole, askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda mkoani Mara wakati wa ibada  ya ufunguzi wa kanisa katoliki Kigango cha Muliaza Parokia ya Butiama leo 03/07/2022. Picha na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi

Mhashamu Baba askofu Simon Masondole askofu wa jimbo katoliki la Bunda amepongeza kitendo cha kizalendo cha Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, kwa kuwa mzalendo na kuchangia maendeleo kwa kujenga kanisa kitendo ambacho kitakuwa daraja litakalowezesha kuvusha wengine katika kuufikia wokovu.

Askofu Masondole amesema hayo Musoma Mkoani Mara wakati akiongoza ibada ya Misa takatifu iliyoambatana na ufunguzi wa kanisa kigango cha Muliaza parokia ya Butiama, kanisa ambalo limejengwa kupitia uwezeshaji wa IGP Sirro, wadau pamoja na watu wengine waliofanikisha ujenzi wa kanisa hilo.

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewapongeza wadau mbalimbali walioshirikiana nae hadi kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo ambapo pia amewataka watu wengine kuendelea kukumbuka mazingira ya nyumbani kwao wanakotoka kwa kusaidia jitihada mbalimbali za kuleta maendeleo.

Ujenzi wa Daraja la Wami kukamilika Agost 31 mwaka huu

 Na Victor Masangu,Chalinze

UJENZI wa mradi wa Daraja jipya la Wami lililopo katika Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani  linatarajiwa kukamilika Agosti 31 mwaka huu ambapo kutakuwa ni mkombozi mkubwa katika kupunguza wimbi la ajali za eneo hilo ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya alipotembelea kukagua ujenzi wa Daraja hilo ambapo limefikia asilimia 93 mradi huo unajengwa na kampuni ya Power Construction Corporation of China Ltd ikisimamiwa na kampuni ya Ilshin Engineers and Advance Solutions Ltd ya Tanzania na limegharimu kiasi cha shilingi bilioni 75.1

Kasekenya alisema kuwa daraja hilo limeghatimu nchi fedha nyingi kwani limejengwa kwa  kutumia teknolojia ya kisasa ambalo lina urefu wa mita 510 likiwa na barabara unganishi kutoka kila upande zenye urefu wa kilometa 3.8 zikiwa zimefikia asilimia 73.

“Ujenzi tumeambiwa unakamilika mwishoni mwa mwezi huu Agosti 31 na tunatarajia magari yaanze kupita Septemba Mosi Mwaka huu na litasaidia kupunguza ajali zilizokuwa zikitokea kwenye daraja la zamani ambalo lilijengwa mwaka 1959,”alisema Kasekenya.

Alisema kuwa ujenzi wa miundombinu unaendelea ambapo serikali ya awamu ya sita inaendelea kusimamia na kutoa fedha kwa ajili hiyo lengo likiwa ni kuifanya nchi kuwa na miundombinu mizuri.

“Kupitia ujenzi wa Daraja hili wataalamu wa hapa nchini wamejifunza teknolojia mpya ambapo asilimia 91 ni wataalamu wa ndani na asilimia tisa ni kutoka nje ya nchi mbali ya kupata utaalamu pia wamejiongezea kipato kupitia mradi huo,”alisema Kasekenya.

Aidha alisema kuwa malengo ya ujenzi wa Daraja hilo ni kukabiliana na changamoto ya ajali, kutumia muda mwingi, uharibu wa mali kutokana na daraja hilo kuwa jembamba na kona kali.

“Hichi ni kielelezo cha Rais bora wa kusimamia miundombinu na haya yalimfanya ateuliwe na bado anaendelea kutuonyesha ujenzi wa miundombinu bora,”alisema Kasekenya.

Naye Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Pwani Baraka Mwambage alisema kuwa lengo la kujenga daraja hilo ni kutatua changamoto zitokanazo na daraja la zamani ambalo halikidhi mahitaji kwani ni jembamba lenye njia moja.

Mwambage alisema kuwa ujenzi huo umetumia Teknolojia ya madaraja marefu na litakuwa na taa za mionzi ya jua zenye kamera 78 ambapo fidia za mali zilizotolewa ni milioni 194.7. Mradi huo ulianza mwaka 2016.