Thursday, November 6, 2014

NBC YAMWAGA ZAWADI KWA WASHINDI WA PROMOSHENI YA WEKA UPEWE

Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Muhimbili, Fatma Gulamsood (kulia) akikabidhi zawadi ya pikipiki kwa mmoja wa washindi wa promosheni ya Weka Upewe ya benki hiyo, Stella Kivuyo katika hafla ya mabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.

Meneja wa Bidhaa za Kuwekeza na Wateja Wakubwa wa Benki ya NBC, Dorothea Mabonye akikabidhi funguo ya bajaji kwa Dk. Nyagosya Range (kushoto), aliyeibuka kidedea katika promosheni inayoendelea ya Weka Upewe ya benki hiyo. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.

HAWA NDIO WATANGAZAJI WALIOTAJWA KUTAKA KUTUMIWA NA IKULU KUURUBUNI MCHAKATO WA KATIBA

Na Karoli Vinsent

             KATIBU mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Dokta Wilbroad Slaa amefanikiwa kupata waraka kutoka ndani ya Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete ambapo Waraka huo umetenga kiasi cha Sh Bilioni 2.5 kwa ajiri ya kuvionga vyombo vya Habari na waandishi na watangazaji ili kuipigia Kampeni Katiba ilyopendekezwa,
       
            Waraka huo ambao mtandao huu unao unawaonyesha watangazaji kutoka Tv mbalimbali nchini, ambao ikulu ya Rais Jakaya kikwete imepanga kuwanunu ili kufanya kazi ya kuongoza vipindi mbalimbali  nyenye lengo la kuwafosi wananchi waipigie kura ya ndio wakati wakuipigia kura katiba iliyopendezwa.
      
               Dokta Slaa aliufichua waraka huo juzi Jijini Dar Es Salaam wakati wa mkutano na waandishi wa Habari Jijini Dar Es Salaam ambapo Kwa mujibu wa Waraka huo kila mtangazaji wa kituo cha TV ambaye ataongoza kipindi kimoja atapewa kiasi cha sh laki mbili (200000) kwa kila kipindi ndani ya wiki 22 yaani katika wiki moja kipindi kitaruka mara mbili kwa wiki na wananchi wataruhusiwa kupiga simu.
       
            Waraka huo umewataja watangazaji wa vituo vya TV ambao watanunuliwa,Natha Chingu ambaye ni Msimamizi wa Vipindi wa redio ya East Afrika ambayo yeye atakuwa mtangazaji wakipindi cha Katiba ndani ya Runinga ya EATV pamoja Samson Charlses kutoka kituo cha Tv EATV,
       
           Kwa upande wa kituo cha Runinga cha ITV ni  watangazaji hao ni Abdallah Mwipaya,Fatuma Shangasa,Ramphedi Mwasako.Wote hao kutoka ITV,
       
            Waraka huo uliwataja watangazaji wengine walionunuliwa kutoka Kituo cha Tv cha Chanel Ten ni David Ramadhani na katika Shirika la Utangazaji la Serika TBC ni Shabani Kissu.
    
             Pia Kituo cha Tv cha Star Tv ni Mzee Angalieni Mpendu na Francic Mawalla na waraka huo umeshindwa kuwataja watangazaji wa vituo vya ZBC pamoja Clauds Tv ambao wamenunuliwa ili kuipigia kampeni katiba iliyopendekezwa,
      

MAKUBWA YAANZA KUIBULIWA SAKATA LA MAKONDA,ELIMU YAKE KUMBE NI----SOMA HAPA

Na Karoli  Vinsent


HUKU ikiwa bado wasomi,wanasiasa na wanaharaki pamoja na taasisi mbalimbali zikiwa zinalaani vikali kitendo cha wahuni waliokodiwa na aliyekuwa Mjumbe wa Bunge Maalum la katiba Paul monda kuvuruga na kupigwa aliyekuwa 

            Mwenyekiti wa tume ya ukusanyaji Maoni ya Katiba mpya Jaji Joseph Warioba wakati mdahalo wa kutoa
  elimu kuhusu katiba iliyopendekezwa na Bunge maalum la katiba,sasa Mapya yaibuka kuhusu Fujo hizo,Mtandao huu unariboti

              Taarifa za kuaminika ambazo Mwandishi wa Mtandao huu amezipata zinasema Chama cha Mapinduzi CCM kilikuwa nyuma za vurugu hizo zilizoibuka wakati wa mdahalo huo wa kutoa elimu kuhusu katiba,na kiongozi wa vurugu hizo ametajwa kuwa ni Paul makonda katibu wa uhamisishaji wa umoja wa Vijana (UV-CCM),
          

Wednesday, November 5, 2014

HABARI KUBWA--MATOKEO YA DARASA LA SABA YAPO HAPA,WENGI WAFAULU

DK. CHARLES E. MSONDE AKITANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA MAPEMA HII LEO OFISINI KWAKE,MSONDA AMESEMA MATOKEO YA MWAKA HUU UFAURU WAKE NI MKUBWA UKILINGANISHA NA  YA MWAKA JANA


Matokeo ya Darasa la 7 kwa mwaka 2014 yametangazwa na Baraza la Mitihani Tanzania Necta ambapo katika matokeo hayo ya mwaka huu yanaonyesha Kiwango cha ufaulu kupanda kwa asilimia 56.99 Tofauti na ufaulu wa mwaka jana ambao ulikuwa Asilimia 51.6 Huku mkoa wa Dar es Salaam ukiongoza.

 HAYA HAPA NDO MATOKEO YENYEWE:

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS




KIKOSI CHA TAIFA STARS KITAKACHOIVAA SWAZILAND HIKI HAPA

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij ametangaza kikosi cha wachezaji 24 kwa ajili ya mechi ya kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) dhidi ya Swaziland itakayochezwa Novemba 16 mwaka huu jijini Mbabane.

Akizungumza Dar es Salaam, leo (Novemba 5 mwaka huu), Nooij alisema kikosi hicho kitaingia kambini Novemba 10 mwaka huu saa 6 mchana kwenye hoteli ya Accomondia, na siku hiyo hiyo jioni kitafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Gymkhana.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA KIMATAIFA LA MITAJI HISA JIJINI DAR ES SALAAM, LEO.

Baadhi ya washiriki wa kongamano hilo waliohudhuri ufunguzi huo wakimsikiliza Makamu wa Rais, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akihutubia. Picha na OMR
- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano hilo mara baada ya ufunguzi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Kongamano la Kimataifa kuhusu Mitaji Hisa, lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta isiyo rasmi ya TPSF, lililofanyika leo Novemba 5, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mwenyekiti wa TPSF, Dkt. Reginard Mengi, wakati alipowasili kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, leo Novemba 5, 2014 kwa ajili ya kufungua rasmi Kongamano la Kimataifa kuhusu Mitaji Hisa, lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta isiyo rasmi ya TPSF.

KUTOKA CHADEMA LEO


Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar Salum Mwalim akihutubia wakazi wa Mji wa Kyela katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya siasa mjini humo . Naibu yuko katika ziara ya siku sita Mkoani Mbeya kukagua maandalizi ya chama kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa Disemba.

Tuesday, November 4, 2014

HABARI HII NAYO HUTAKIWI KUIKOSA

1
Rais wa tuzo za TWA Irene Kiwia akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye hoteli ya Serena  jijini Dar es salaam wakati akielezea maandalizi ya tuzo hizo kwa mwaka huu wa 2014, Katikati ni Mwenyekiti wa tuzo za TWA mama Sadaka Gandi na kulia ni Hellen Kiwia katibu TWA.

VURUGU MDAHALO WA WARIOBA--WANAHARAKATI WACHARUKA,SOMA KILICHOZUNGUMZWA MUDA HUU JIJINI DAR ES SALAAM

Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC Bi HELLEN KIJO BISIMBA akizungumza na wanahabari muda huu katika ofisi za makao makuu ya kituo hicho kijitonyama jjni dar es salaam,kushoto kwake ni  mkurugenzi msaidizi wa JUKATA ndugu HEBRONI MWAKAGENDA
Ikiwa ni siku kadhaa kupita tangu tukio la kufanyiwa fujo kwa mdahalo ulikuwa unafanyka jijini Dar es salaam chini ya mwenyekii wa tume ya mabadiko ya katiba Tanzania jaji JOSEPH SINDE WARIOBA, asasi mbalimbali  za kiraia wameibuka na kauli nzito ya kulaani kitendo hicho ambacho wamedai kuwa kinafedhehesha taifa.

Wakizungumza na wanahabari muda huu jijini Dar es salaam wanaharakati hao wakIongozwa na mkurugnzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu Bi HELLEN KIJO BISIMBA wamesema kuwa kitendo cha kuvuruga mdahalo huo ni kitendo cha kulaaniwa na kila mtanzania mpenda haki na si kitendo kizuri katika mchakato wa kupata katiba ya Tanzania. 
Wanahabari wakiwa wanafwatilia kwa umakini 

          “ndugu wanahabari kitendo cha kufanya vurugu katika mdahalo wa juzi kinapaswa kulaaniwa na kukemewa na kila mwananchi mwenye mapenzi mema na taifa la Tanzania na hasa viongozi wananchi wenye dhamana yakulinda na kutetea democrasia na amani tuliyo nayo.amesema bi HELLEN.

           Aidha amesema kuwa vurugu hizo zimeonyesha kuwa zina lengo la kuwatisha wanachi wasijadili katiba waitakayo kwa muskatabali wan chi yao,ambapo amesema kuwa ni lazima kitendo hiki kikemewe na kila mtanzania ili kuweza kuweka dmocrasia ya kweli katia kutoa maoni ya katiba ya Tanzania.
         Katika hatua nyingine wanaharakati hao wamvitaka vyombo vya  sheria kuhakikisha kuwa wanawatia mbaroni vijana wote walioonekana kuanzisha vurugu hizo juzi katika mdahalo huo kwani kuna njia nyingi za kuwakamata ikiwa ni pamoja na kutiza mikanda ya video ambayo imerekodiwa aidha na uongozi wa ukumbi huo au wanahabari. 
 mkurugenzi mstaafu wa chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA bi ANANILEA NKYA akizungumza na wanahabari jijini dar es salaam

Monday, November 3, 2014

HABARI ILIYOTIKISA JIJI--PAUL MAKONDA AIBUKA ,AJIBU TUHUMA ZA KUDAIWA KUMPIGA JAJI WARIOBA--SOMA HAPA


Na Karoli Vinsent
SIKU moja kupita Baada ya  aliyekuwa  Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba,  Paul Makonda kumrushia Chupa aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya ukusanyaji Maoni ya Katiba  Jaji Joseph Warioba wakati wa mdahalo wa kutoa elimu kuhusu Katiba iliyopendekezwa na bunge Maalum la Katiba

TAMASHA LA TIGO WELCOME PACK LAFUNIKA MJINI MOSHI--PICHA ZOTE ZIKO HAPA

Wasanii wakundi la Original  Komedi wakitoa burudani kwenye uwanja waUshirika Mjini Moshi wakati wa kampeni ya kifurushi  cha Tigo we lcome pack, Kifurushihichokitamwezesha mtumiaji wa Tigo kupata muda wa maongezi wa dakika  20, mb175,sms bila kikomo na pesa shilingi mia 500 kwenye akaunti yake ya tigopesa, yote hayo kwa shilingi 1000 mteja atakaponunua laini yake yaTigo

Sehemu ya umati uliofurika kwenyeTamash la Tigo welcome pack uwanja wa Ushirika Mjini Moshi.

. Msanii  Emmanuel Mgaya Maarufu Masanja Mkandamizaji akiwapa raha wa kazi wa Moshi waliofurika kwenye uwanja wa Ushirika wakati wa onesho la Tigo welcome pack
Msanii Ibrahim Mussa maarufu Roma Mkatoliki akipiga shoo kwenye tamasha la Tigo welcome pack uwanja wa Ushirika mjini Moshi mwishoni mwa wiki.

Msanii Slivery Mujuni maarufu Mpoki akiwapa burudani wakaziwa Moshi waliofurika kwenye uwanja wa Ushirika hii ni sehemu ya burudani zitolewazo kwenye kampeni ya kifurushi kipya  cha Tigo cha welcome pack.


Sunday, November 2, 2014

TIZAMA PICHA ZA WARIOBA AKIOKOLEWA JANA KWENYE VURUGU UBUNGO



Pichani ni Mzee Warioba akitolewa nje baada ya vurugu zilizojitokeza katika Mdahalo wa "Mchakato wa Katiba Mpya, Maoni ya Wananchi na Katiba Inayopendekezwa" yaliyofanyika mapema jana hii Ubungo Plaza. 

HAYA NDIYO YALIYOJIRI UBUNGO KWENYE MDAHALO,MAKONDA AMTWANGA WARIOBA MCHANA KWEUPE


Jaji Warioba.

VURUGU zilizoambatana na ngumi kurushwa zimetokea hivi punde katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam wakati aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba alipokuwa akitoa mada kwenye mdahalo wa kujadili umuhimu wa kuielewa kwa kina Katiba inayopendekezwa kama ilivyopitishwa na Bunge Maalum la Katiba.
 
Vurugu hizo zimezuka baada ya watu waliokuwa na mabango kuvamia ukumbuni hapo na kusababisha baadhi ya watu waliokuwa wanafuatilia mdahalo huo kuwakabili na kuwapa kichapo.
 Baada ya vurugu hizo, mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kurushwa moja kwa moja na ITV umesimamishwa kwa muda.

Kwa upande wake Gwiji La masuala ya habari nchini na Mhariri wa Gazeti la Tanzania Daima Edson Kamukara alichukizwa na kitendo cha Makonda haya ndio aliyoyasema kwenye ukrasa wake facebook


SOMA ZAIDI WALICHOKISEMA WADAU JUU YA YUKIO HILO LA TUHUMA ZA MAKONDA KUMPIGA WARIOBA NA CHUPA