Nundu ameangushwa na mpinzani wake mkubwa wa siasa, ambaye aliwahi kuwa Meya wa Jiji la Tanga, Salim Kassim Kisauji, aliyeshinda kwa kupata kura 514. Kura hizo, zilipigwa mara mbili, baada ya awamu ya kwanza kukaribiana kwa karibu na Saumu Bendera, aliyepigiwa kura 446.
KOROGWE VIJIJINI
Habari kutoka Korogwe Vijijini, zinasema, Mbunge wa jimbo hilo, Stephen Ngonyani maarufu (Profesa Majimarefu), ameangukia pua, baada ya kushindwa na mpinzani wake, mchumi Dk. Edmund Mndolwa.
No comments:
Post a Comment