
Mechi
zote saba zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni ambapo Yanga na Simba zitakuwa
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa mechi ambayo viingilio vyake ni sh. 7,000
kwa viti vya bluu na kijani, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000
kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 30,000.
Tayari
tiketi zimeanza kuuzwa leo (Aprili 18 mwaka huu) katika vituo saba vya; Shule
ya Sekondari Benjamin Mkapa, Kariakoo (Kidongo Chekundu), Buguruni Shell,
mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Ohio na Samora, Ubungo OilCom, Dar Live
Mbagala na Uwanja wa Taifa.
Mechi
nyingine zitakuwa kati ya Tanzania Prisons na Ashanti United (Uwanja wa
Jamhuri, Morogoro), Rhino Rangers na Ruvu Shooting (Uwanja wa Ali Hassan
Mwinyi, Tabora), Mbeya City na Mgambo Shooting (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Oljoro
JKT na Mtibwa Sugar (Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha) na Coastal
Union na Kagera Sugar (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga).
No comments:
Post a Comment