Lema ana ari kubwa ya mapambano. Anasikitishwa Sana na ukiukwaji mkubwa wa Haki na mahakama kuonekana kuendeshwa na Serikali. Yeye ameona Ni bora akae ndani Mpaka hapo Dola itakapopenda kumpa dhamana. Kosa lake lina dhamana na hakimu alimpa dhamana.
Ameomba tutazame mahabusu wengi wanaokaa ndani miaka Mingi bila kesi zao kuendelea. Tuwatetee.
Amemshukuru Mungu Kwa kumpa Mke jasiri anayempa moyo na Ndio ngome yake Kwa sasa.
Nimemwomba Lema aone kuwa hii struggle sio yake peke yake bali anawakilisha watu wengi wanaotaka Haki kutendeka Katika uendeshaji wa Nchi yetu. Siku zote Haki hushinda

Leo December 2 2016 Mahakama kuu kanda ya Arusha imetupa rufaa ya kupinga maamuzi ya kumnyima dhamana iliyoamuliwa na mahakama ya hakimu mkazi dhidi ya mbunge wa Arusha mjini Godbles Lema.
Naibu msajili wa Mahakama kuu kanda ya Arusha, Anjelo Rumisha amesema kwamba rufaa hiyo ilikuwa imekatwa nje muda uliopangwa.
No comments:
Post a Comment