Wednesday, October 25, 2017

WANAHARAKATI WA GDSS WAPEWA ELIMU YA KUPATA MIKOPO YA 10% ZA KILA HALMASHAURI

TGNP Mtandao ni miongoni mwa mashirika makongwe yaliyokuwa yakipigania vuguvugu la ukombozi wa wanawake, na kwa kuliona hilo serikali ya Tanzania ikatoa agizo kwa kila halmashauri kutenga asilimia 5 wa ajili ya wanawake na asilimia 5 nyingine kwa ajiri ya vijana.
Hayo yamesemwa mapema jana na muwezeshaji wa semina ya jinsia na maendeleo bi. Bertha s.masagasi ambae ni afisa maendeleo wa jamii wa manispaa ya ilala alipokuwa akitoa elimu kwa wanaharakati mbalimbali kuhusu mfuko wa WYDF unaopatikana katika kila halmashauri hapa nchini.

Muwezeshaji huyo alisema kuwa mfuko huu ulianzishwa mnamo mwaka 1993 wa uwezeshaji wanawake na vijana na ulianza utekelezaji wake mwaka huo huo kwa mikoani mingine, lakini kwa halmashauri za jiji la Dar es salaam zilianza kutenga fedha hizo ikiwa ni utekelezaji wa agizo hilo mwaka wa fedha 1998/99.
Lakini pia kwa Tanzania inaonyesha kuwa tumepiga hatua zaidi kwa swala la uwezeshaji na mpaka sasa kuna mifuko 19 na iliyopo katika serikali za mitaa yetu ni mitatu.

Kundi la kwanza ni la vijana ambalo mfuko wake upo chini ya wizara ya kazi na maendeleo ya vijana, na kundi la pili ni la wanawake ambalo msimamizi wake ni Wizara ya Afya Jinsia Maendeleo Wazee na Watoto, na kundi la mwisho la uwezeshaji wanawake na vijana ambalo lipo chini ya Halmashauri.

Na inaonyesha kuwa mfuko huu wa halmashauri haukuwapa nafasi sana wanaume na kuwapendelea zaidi wanawake kwa kuwa mwanaume anapzaliwa tayari ameshawezeshwa hivyo ana changamoto nyingi kama mwanamke, ndio maana umri wa vijana umewekwa ni miaka 18-35 na wanawake kuanzia miaka 18 mpaka 60.
Hata hivyo imeonekana kuwa wanawake wengi hawakaopesheki katika mabenki kwa kuwa hawana cha kuweka rehani kama nyumba, mashamba nk. Lakini pia wanawake hao wana mzigo mkubwa wa majukumu anapoipata fedha hiyo ambapo itatumika kwenye chakula au shida yoyote nyumbani na matokeo yake atashindwa kurudisha marejesho ndio maana mfuko huo umewapa nafasi kubwa wanawake hao.

Aidha muwezeshaji huyo aliendelea kusema kuwa kituo kinakuwa na watu 50 ambao wamejigawa katika vikundi vya watu 10 na masharti yake ni kuchukua kuanzia laki 2 au chini ya hapo lakini ukomo wake ni milioni 5, na hii ni kwa usimamizi wa serikali za mitaa na kata kwa kuleta taarifa sahihi za wakazi wake ili isije kutokea hali ya sintofahamu na fedha kupotea bure.
Lakini pia dada bertha aliendelea kusisitiza kuwa ili kuendana na sera ya serikali awamu ya tano yakuwa na uchumi wa viwanda wao wameitumia fursa hiyo na kuongezea kuwa ni viwanda na uchuuzi, kwani wakopaji sio wote ni wazalishaji ama wachakataji lakini kuna madereva wa boda boda, wamachinga, wauza maji, wanawake wabeba mabeseni nk. Hawa wote wanatakiwa kuwezeshwa na mikopo hiyo.


Na mwisho alimalizia kwa kusema kuwa wanafanya kazi na mashirika kama SIDO, VETA, TFDA, UNIDO nk. Kwa kuwasaidia wajasilimali wadogo wadogo wanapozalisha ama kuchakata bidhaa zao ziwe na kiwango cha kimataifa ili kuweza kuuzika hata nje ya nchi na hata kupata masoko katika supermarket kubwa hapa nchini.

No comments: