Bonasi Kemkem Kwa Wateja Wa
Tigo Watakaonunua Bando Kupitia *147*00# Pata hadi GB 1 bure na nafasi ya
kushinda simu janja ya 4G kila saa!
Kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali
Tigo Tanzania leo imetangaza promosheni murwa kwa wateja wake wote watakaonunua
bando za data kuanzia TZS 1,000 kupitia menu iliyoboreshwa ya *147*00#,
ambapo watapokea bonasi ya hadi 1GB bure papo kwa hapo kwa matumizi
ya Facebook, WhatsApp, Instagram ama Twitter.
Pamoja na haya, wateja hao pia watapata nafasi ya kushinda
mojawapo ya simu janja zenye uwezo wa 4G aina ya TECNO R6 zaidi ya elfu moja
ambazo zinatolewa na Tigo katika promosheni hiyo kabambe ya ‘Nyaka Nyaka
Bonus’.
Akitangaza ofa hizo jijini Dar es Salaam leo, Afisa Mkuu wa
Biashara wa Tigo, Tarik Boudiaf alisema kuwa ofa hizo murwa ni sehemu ya
ubunifu wa Tigo unaolenga kukutana na mahitaji ya wateja na kuwezesha kila mtu
afurahie huduma za kidigitali katika mtandao ulioboreshwa wa Tigo.
“Kupitia mtandao wetu
mathubuti wa 4G wateja wetu tayari wanafurahia huduma bora zaidi za intaneti.
Promosheni ya Nyaka Nyaka Bonus inatoa fursa kubwa kwa wateja wengi zaidi
kumiliki simu janja zenye uwezo wa 4G na kupokea bonasi kubwa za data
zitakazowawezesha kuwa sehemu ya mageuzi makubwa ya kidigitali yanayoongozwa na
Tigo,’ alisema.
Tigo ndio mtandao
unaoelewa zaidi mahitaji ya wateja wake ambapo katika soko la simu za mkononi
nchini, ni wateja wa Tigo pekee wanaopokea bonasi za bure kwa kila kifurushi
wanachonunua. Tigo pia imejizolea umaarufu mkubwa kwa promosheni zake bunifu.
Kwa upande wake,
Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo, Simon Karikari alisema kupitia promosheni mpya ya
Nyaka Nyaka Bonus, Tigo inalenga kuongeza matumizi ya data pamoja na kuongeza
matumizi ya simu janja za kisasa (Smartphone) nchini, hivyo kuisogeza Tanzania
hatua moja mbele zaidi katika ulimwengu wa kidigitali.
‘Tunafahamu kuwa idadi
kubwa ya Watanzania bado hawajafikiwa na huduma za mtandao na ndio maana Tigo
inazidi kuwekeza katika kupanua na kuboresha huduma zake za mtandao. Kupitia
promosheni hii tunalenga kuongeza idadi ya watumiaji wa simu za kisasa pamoja
na matumizi ya data nchini,’ alisema.
“Tunawakaribisha wateja wetu wote kuchangamkia
fursa hii kwa kununua vifurushi vya data vya kuanzia TZS 1,000 kupitia menu
yetu ya *147*00# ili waweze kufaidi bonasi za papo hapo za intaneti kwa
matumizi ya mitandao ya jamii kama vile Facebook, WhatsApp, Instagram ama
Twitter. Vile vile, kila kifurushi wanachonunua kitawaingiza katika droo ambapo
watapata nafasi ya kushinda mojawapo za zaidi ya simu janja 1,000 aina ya TECNO
R6 yenye uwezo wa 4G ambazo Tigo inatoa katika msimu huu,” Tarik alisisitiza.
No comments:
Post a Comment