Friday, December 5, 2014
WAZIRI MWAKYEMBE AWAPONGEZA FASTJET KWA HUDUMA BORA KWA WATEJA WAKE
TIGO,VODACOM,NA AIRTEL ZASHIRIKIANA NA "AU" KUTOKOMEZA EBOLA AFRICA
Kampuni za simu nchini Tanzania zimeingia katika
ushirikiano na Tume ya Umoja wa Afrika (AU Commission) ili kuendeleza vita
dhidi ya ugonjwa wa Ebola unaoendelea kutishia amani nchi za Afrika Magharibi.
Ushirikiano huo unaojulikana kama ‘AfricaAgainstEbola’(AfrikaDhidiYaEbola)itatumia
mtindo wa ujumbe wa kiganjani (SMS) kuweza kuchangisha fedha kwa ajili ya
kuwawezesha watalaam wa afya kutoka Afrika kuweza kwenda na kuhudumia nchi
zilizo athirika.
Watu
zaidi ya 5,000 wameshapoteza maisha kutokana na ugonjwa wa Ebola kutoka sehemu
mbali mbali Afrika Magharibi tangu ugonjwa huo kulipuka kwa mara ya kwanza
nchini Guinea mwezi Machi 2014. Kutokana na taarifa za Shirika la Afya Duniani
(WHO) huu ni mlipuko mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika bara hili ambayo kwa
sasa ugonjwa huo umeshatapakaa katika nchi nne zikiwemo – Guniea, Liberia,
Sierra Leone na Mali.
Katika
mkutano wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni chini ya AU, kampuni za simu
zilijitolea kuanzisha kampeni maalum ya bara nzima ijulikanayo kama “United Against Ebola” (Pamoja Dhidi ya
Ebola). Kampeni hii itakusanya michango kutoka kwa wateja wa kampuni mbali
mbali za simu, na fedha hizo zitakazo kusanywa katika muda wa miezi mitatu,
zitatumika katika mapambano dhidi ya kirusi hiki cha Ebola.
ZITTO ATOA SHARTI MOJA ILI AREJEE CHADEMA,SOMA HAPA
Harufu ya kuisha kwa mgogoro baina ya Zitto Kabwe na
chama chake cha Chadema inanukia, lakini mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini
anataka kuwapo na mazungumzo kubaini tatizo ili atakayebainika kuwa
alifanya makosa awe tayari kuomba radhi hadharani.
Zitto alikiri bungeni kuwa amekuwa “akimiss” harakati zilizokuwa
zikifanywa na vyama vya upinzani wakati wa Bunge Maalumu la Katiba,
harakati zilizozaa Umoja wa Katiba ya Wananchi na kufurahia kuhudhuria
kwa mara ya kwanza vikao vya umoja huo.
Zitto, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali
(PAC), alipata fursa ya kuingia vikao vya Ukawa wakati wapinzani
walipoungana tena kupambana dhidi ya wizi wa fedha kutoka Akaunti ya
Tegeta Escrow, sakata ambalo liliwekwa bayana na kamati yake baada ya
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila kulifikisha bungeni, lakini
hakudokeza lolote kuhusu Chadema.
ESCROW UPYAAA--KAFULILA ALIPUKA TENA,SASA NI IKULU LAWAMANI,SOMA ALICHOKISEMA MUDA HUU
WAKATI Rais Jakaya Kikwete akisuasua
kuwachukulia hatua viongozi waliotajwa na Bunge kuhusika Katika Wizi wa zaidi
ya Bilioni 320 kwenye Akaunti ya Tegeta Esrcow ,naye Mbunge wa Kigoma Kusini
David Kafulila Ameibuka upya na Ameivaa Ikulu
Baada ya kusema Ikulu ya Rais Jakaya
Kikwete inamedhamilia kuwalinda wezi waliohusika katika kuiba pesa hizo,baada ya
kumzuia Mkurugenzi wa ofisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa PCCB Dk Edward
Hosea kutoiwasilisha Taarifa ya uchunguzi juu ya sakata hilo la Esrcow kwa Umma kutokana na Ripoti ya PCCB kuwataja
vigogo wa Ikulu kuhusika katika kuchota pesa kwenye Benk ya Stabink.
HABARI PICHA--TESEMA FC YA KINONDONI YAJIPIMA UBAVU NA MTIBWA SUGAR KARUME
Thursday, December 4, 2014
TASWA YAPITIA MAJINA YA WATU WALIOTANGAZWA KUWANIA TUZO,YOTE YAKO HAPA
KAMATI ya Kusimamia Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania zinazotolewa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) ilikutana Dar es Salaam jana na kupitia majina ya wanamichezo waliopendekezwa kuwania tuzo hizo.
Tuzo itafanyika Desemba 12 mwaka huu ukumbi wa Diamond, Jubilee (VIP), Dar es Salaam, ambapo wanamichezo mbalimbali waliofanya vizuri kati ya Juni 2013 hadi Juni 2014 watakabidhiwa tuzo zao.
Ni imani yetu kwamba zaidi ya wanamichezo 40 watakabidhiwa tuzo zao siku hiyo, ambapo kamati imejiridhisha kwamba wanaowania tuzo hiyo wanastahili kulingana na mapendekezo ya vyama vya michezo kupitia Kamati zao za Ufundi.
Mshindi wa kila tuzo ataingia katika mchakato wa kumpata Mwanamichezo Bora wa Tanzania wa mwaka 2013/2014, ambapo pia siku hiyo ya sherehe za tuzo itatangazwa zawadi ya Tuzo ya Heshima kwa yule ambaye itaonekana alikuwa na mchango mkubwa katika masuala mbalimbali ya kimichezo hapa nchini. Tuzo hizo ni kuanzia Juni 2013 hadi Juni 2014.
ORODHA KAMILI YA WANAOWANIA TUZO ZA TASWA 2013/2014
KAMISHNA KOVA AWATAKA ASKARI WALIOMALIZA MAFUNZO YA UONGOZI MDOGO WA JESHI LA POLISI KUTUMIA UJUZI NA MAARIFA WALIYOYAPATA KUONDOA KERO NA KUDUMISHA AMANI KATIKA MITAA YOTE YA JIJI LA DAR
![]() |
| Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Kipolisi ya Dar es Salaam,Kamishna Suleiman Kova akifurahi jambo wakati akizungumza na Askari Polisi waliomaliza Mafunzo ya uongozi mdogo wa Jeshi la Polisi katika vyuo vya Polisi vya Moshi na Zanzibar,wakati alipowapokea leo Desemba 4,2014 katika Kituo cha Kati cha Polisi,Jijini Dar es Salaam. |
![]() |
| Sehemu ya Askari Polisi waliomaliza Mafunzo ya uongozi mdogo wa Jeshi la Polisi katika vyuo vya Polisi vya Moshi na Zanzibar wakimsikiliza Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Kipolisi ya Dar es Salaam,Kamishna Suleiman Kova,wakati akiwaasa maswala mbali mbali yahusuyo Jeshi hilo. |
![]() |
| Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam amewapokea askari waliomaliza mafunzo ya uongozi mdogo wa Jeshi la Polisi katika vyuo vya Polisi vya Moshi na Zanzibar ambao ni utaratibu wa kawaida na kuwaasa mambo yafuatayo: |
KUELEKEA SIKUKUU HIINDIO KAULI YA SUMATRA JUU YA USAFIRI WA MIKOANI
![]() |
| Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafi wa nchi kavu na Majini, Dk Oscar Kikoyo akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es salaam jana juu ya hali ya usafiri kipindi cha siku kuu za Krismas na mwaka mpya ambapo ametahadharishja abiria kuto kukubali kutozwa nauri za juu na pindi ikitokea hivyo Sumatra ipewe taarifa haraka.
BARAZA
la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa nchi Kavu na Majini
(SUMATRA Limewakumbusha wamiliki wa Mabasi yaendayo Mikoani na
Madereva kufuata Masharti ya Leseni zao kwa kutotoza nauli kubwa
katika kipindi hiki cha Sikuku za mwezi Desemba na endapo mtu akikiuka
sheria basi Mamlaka hiyo haitosita kumfutia Leseni ya Basi
litakalokwenda kinyume.
|
TIZAMA WALICHOKIFANYA CHADEMA KWENYE BUNGE LA ULAYA
fastjet kwenye maadimisho ya miaka 70 ya kimataifa ya safari za anga duniani
OFisa Habari na Masoko wa Fastjet, Lucy Mbogoro, (kulia), akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dr.Shaaban Mwinjaka katika maadhimisho ya miaka 70 ya Kimataifa ya safari za Anga Duniani yaliyoanza jana mpaka Desemba 5 mwaka huu katika Viwanja vya Makao Makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCCA) Dar es Salaam, kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TCCA, na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Charles Chacha.
TAARIFA MAALUM KWA WATEJA WA NBC KUHUSU PESA ZAO
Wednesday, December 3, 2014
CHADEMA WAPATA MWALIKO BUNGE LA ULAYA,SOMA HAPA
| Baadhi ya viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo
CHADEMA wamepata mwaliko wa kuhudhuria Bunge la ulaya nchini Ubelgiji,
na kukutana na viongozi wa bunge hilo, pamoja na kuhudhuria mkutano Mkuu
wa 27 wa chama cha CDU nchini Ujerumani. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Kaimu katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalim amesema, ujumbe huo wa CHADEMA utafanya mazungumzo na viongozi wa bunge hilo, juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea hapa nchini. Amesema kama chama kikuu cha upinzani, watakaowakilisha ni ujumbe wa viongozi wakuu wa Chadema na wamejipanga kufanya mazungumzo, maalumu kwa mustakabali wa taifa la Tanzania. Aidha mwalimu amesema wakiwa nchini ujerumani viongozi hao watazungumzia changamoto mbalimbali zinazolikabili taifa Ujumbe huo wa CHADEMA tayari umeshaanza safari yake, na utakuwa kwenye ziara hiyo kwa muda wa siku kum |
Subscribe to:
Posts (Atom)















