Wednesday, September 3, 2014

michezo--MECHI ZA KIMATAIFA ZA KIRAFIKI..ROONEY NA DI MARIA WATISHA USIKU HUU,TIZAMA HAPA


Nahodha babu kubwa; Wayne Rooney akipongezwa na wenzake baada ya kufunga bao pekee usiku wa leo
NAHODHA wa England, Wayne Rooney ameitendea haki beji katika mchezo wake wa kwanza tangu arithi mikoba ya Steven Gerrard aliyestaafu, baada ya kufunga bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Norway Uwanja wa Wembley usiku huu.


Nahodha huyo wa Manchester United pia, alifunga bao hilo pekee kwa mkwaju wa penalti dakika ya 68, kufuatia nyota wa Liverpool, Raheem Sterling kuchezewa rafu kwenye eneo la penalti.

Katika mchezo huo uliohudhuriwa na watu 40,181 – idadi ndogo zaidi ya mahudhurio kwenye Uwanja wa Wembley tangu ufunguliwe tena, kinda Sterling alizawadiwa heshima ya mchezaji bora mechi baada ya kazi nzuri kwenye kikosi cha Roy Hodgson usiku wa leo

Kifaa halisi; Angel di Maria ameng'ara vilivyo leo Argentina ikilipa kisasi cha Kombe la Dunia kwa Ujerumani 


WINGA Angel di Maria ametengeneza mabao matatu na kufunga moja, Argentina ikilipa kisasi cha Kombe la Dunia kwa kuifunga 4-2 Ujerumani usiku huu katika mchezo wa kirafiki mjini Dusseldorf, Ujerumani.

Mchezaji huyo ghali zaidi kuwahi kusajiliwa Manchester United na Uingereza nzima alipika mabao ya Sergio Aguero, Erik Lamela na Federico Fernandez kabla ya kufunga na lake mwenyewe siku 52 tangu bao la Mario Gotze katika muda wa nyongeza liipe Ujerumani ubingwa wa dunia nchini Brazil.

Mabao matano kati ya sita yamefungwa na wachezaji wa Ligi Kuu ya England, huku Andre Schurrle akiifungia Ujerumani kabla ya Gotze kuwafungia bao la pili mabingwa hao wa dunia. 

BUNGE MAALUM LA KATIBA LEO KATIKA PICHA

PIX 6.Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta (kulia) akiteta jambo na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru wakati wa Bunge Maalum la Katiba leo 03 Septemba, 2014 Mjini Dodoma.
PIX 7,PIX 2.Baadhi ya Wajumbe toka Kamati mbalimbali wakiendelea kuwasilisha taarifa za Kamati zao katika Bunge Maalum la Katiba leo 03 Septemba, 2014 Bungeni Mjini Dodoma.

KUHUSU TAARIFA ZA KUPIGWA RISASI MWANDISHI SAID KUBENEA,UKWELI NDO HUU

Na Karoli Vinsent

    KUFUATIA taarifa mbalimbali zilizokuwa zimezushwa na kusambazwa kwenye simu pamoja na Mitandao ya kijamii kwamba Mwandishi Mwandamizi na Mzalendo wa Nchi yake, Saed Kubenea amepigwa Risasi na hali yake kuwa mbaya,sasa hivi ndivyo  mwenyewe alivyojibu
      
          "Taarifa zimetupwa kwenye mitandao ya simu, zikisema kuwa mimi Saed Kubenea, nimejeruhiwa kwa risasi na kwamba hali yangu ni mbaya sana. Imeelezwa kuwa tukio hilo lilitokea leo majira ya saa tano asubuhi katikati ya jiji la Dar es Salaam.


    Binafsi nimejulishwa tukio hilo na Mwandishi wa habari wa Star TV na baadaye nikaelezwa kuwapo uvumivu huo na Katibu wa Jukwaa la Wahariri, Neville Meena.
Napenda kuujulisha umma kuwa habari hizo siyo kweli. Mimi niko salama na naendelea na majukumu yangu kama kawaida”alisema Kubenea

     Ikumbukwe Kubenea ni Mwandishi wa Gazeti la Mawio na mmiliki  , MwanaHALISI Online.com na mtandao wa MwanaHALISI Forum pamojaMkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Hali Halisi Publishers Limited - wachapishaji wa gazeti la MwanaHALISI, lilosimamishwa na serikali kwa muda usiojulikana, MSETO,ambapo kubenea ambaye amefungua kesi Mahakama kuu kushinikiza Bunge Maalum la Katiba livunjwe kutokana na bunge hilo kupoteza pesa za Watanzania


Microsoft Windows Phone 8.1yatambulishwa Tanzania kupitia Lumia 930, Lumia 630 and Lumia 530

Meneja mawasiliano wa microsoft mobile divice akizungumzia uzinduzi huo
 KAMPUNI ya Microsoft leo imetambulisha aina tatu ya Lumia ambazo ni Lumia 530, Lumia 630 pamoja  na Lumia 930 huku zikiwa zimeunganishwa kabisa na mfumo mpya na wa kisasa wa kiteknolojia wa uendeshaji wa simu wa Windows Phone 8.1.

Mfumo huo mpya wa Windows Phone 8.1 unatoa mwanya zaidi kwa watumaiji wa simu hizo kuhakikisha kuwa wanajiunganisha na huduma mbalimbali za kisasa hasa katika lumia 530.

Pia kupitia mfumo huo wataalamu wa masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wanakuwa na mwanya mpana zaidi wa kuweza kujitengenezea bidhaa mbalimbali za kiteknolojia kupitia hiyo Window Phone 8.1.
Meneja wa bidhaa wa Microsoft, Kingori Gitahi akizungumza wakati wa kutambulisha huduma hiyo mapema leo jijini Dar es salaam
 Meneja wa bidhaa wa Microsoft, Kingori Gitahi alisema kuwa  kupitia bidhaa hizo mtumiaji anakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi kutumia huduma kama vile za mawasiliano ya moja kwa moja kwa njia ya Skype na zile za Microsoft Office.

      Alisema kuwa watumiajiwasimuhizowanakuwanawakatimzurizaidikatikakujipatia huduma za uhakika za mitandao ya kijamii kama vile Instagram, WhatsApp, Viber na WeChat.

      Aliongeza kuwa inamfumomzurizaidiwamatumiziyaKamera kwa kiwango kikubwa cha 5MP huku ikiwa ni rahisi kuunganishwa kwa matumizi ya huduma za laini mbili za simu.
       
      "Pia ina kadi yenye ukubwa wa 4GB ambayo inayoweza kuunganishwa na kuongeza uwezo wake wa kazi kupitia kadi ya hadi kiwango cha 128GB," alisema Kingori.
      Aliongeza kuwa " pia kwa kupitia mfumo huo wa Microsoft pia mtumiaji anajipatia zaidi kiwango cha15GB ambapo mtumiaji huyo atakuwa kwenye wakati mzuri wa kutumia huduma hizo akiunganishwa na computers, laptops na tablets".
 Aliongeza kuwa kupitia bidhaa ya Lumia 630 mteja anakuwa na uwezo wa kupata huduma za Nokia Mapambazo inamwezesha wapi anaelekea na wapi anatokea.

Alisema kuwa hali hiyo inasaidia kwa kiasi kikubwa mteja kufurahia huduma mbalimbali za Nokia Map huku akiwa na wakati mzuri wa kuweza kubabilisha rangi ya muonekano wa simu yake.

Alifafanua kuwa katika simu za Nokia 930 kuna huduma mbalimbali ikiwamo inayomwezesha mteja kujua ni kiwango cha matembezi aliyotembea, amepungua kilo ngapi ikiwa pamoja na kumwelezea umbali wa kiwango alichotembea.

Alisema kuwa ina kiwango kikubwa cha kurekodia Video huku ikiwa na uwezo mkubwa wa kuchuja sauti na kurekodi vizuri zaidi.

 Alisema ina wireless charge uwezo mkubwa wa picha kwa umakini kama camera ya kawaida ikiwa na kiwango cha 1080p Full HD huku ikiwa na betrii yeye uwezo mkubwa wa kuhifadhi umeme  kwa kiwango cha hali ya juu.

Aliongeza kuwa aina hizo zote za Nokia Lumia zina huduma ya bure ya hera Map ambapo mtumiaji anaweza kujua ni wapi alipo wapi aendako pia.

Alisema kuwa ni fursa nzuri kwa mtumiaji hasa mtalii kujua huduma aitakayo katika mahala alipo, huduma kama vile migahawa, benki na nyinginezo ambapo kupitia huduma ta Here Map mtumiaji anaweza kupata hadi namba za simu za watoa huduma husika inayotafutwa.

Alisema kuwa kwa sasa bidhaa hizo zinapatikana kwa bei tofauti ambapo lumia 530 ni Shilingi 240,000, Lumia 630  inauzwa shilingi 345,000 huku Lumia 930 ni shilingi 1,200,000.

Tuesday, September 2, 2014

AMKA NA MICHEZO--TIZAMA JINSI KLABU ZA ENGLAND ZILIVYOFANYA KUFURU YA USAJILI MSIMU HUU


Am I worth it? Angel di Maria was the most expensive acquisition after joining United for a record £59.7m


Mimi ni bosi wao? Angel di Maria amekuwa mchezaji aliyenunuliwa kwa bei mbaya zaidi kihistoria Uingereza baada ya Manchester United kulipa Pauni Milioni 59.7 Real Madrid

 KLABU za Ligi Kuu ya England zimetumia Pauni Milioni 858 baada ya dirisha la usajili msimu huu kufungwa, ambayo ni zaidi ya kiasi kilichotumika kwa klabu za La Liga ya Hispania (Pauni Milioni 425), Serie A ya Italia (Pauni Milioni 260) na Ligue 1 ya Ufaransa (Pauni Milioni 100) jumla.

Hii imeipiku hata Ujerumani ambako klabu zilipoamua kuingia sokoni kwa fujo Bundesliga zilitumia Pauni Milioni 250 jumla pamoja na Pauni Milioni 100 kwa awamu moja ya usajili.

Sehemu kubwa ya fedha inatokana na mikataba ya Televisheni England ambayo inazipa jeuri klabu kusajili kwa bei kubwa na kulipa mishahara minono wachezaji. 



Chati hii inaonyesha namna klabu zilivytumia fedha kusajili Ulaya, Ligi Kuu England ikiongoza kwa kutumia Pauni Milioni 857.68

FEDHA NYINGI ZIMEKWENDA KWA WACHEZAJI WA KIGENI

FAHAMU ALICHOKIFANYA KAMISHNA KOVA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam SULEMAN KOVA leo akionyesha aina ya silaha ambazo zimekamatwa ndani ya jiji la Dar es salaam kwa wiki hii ambapo amesema kuwa ni harakati za kulifanya jiji la dar es salaam liwe salama na amani itawale ndani ya jiji hili.

Kamishna kova ameendelea kutoa onyo kwa watu ambao wanafanya uhalifu kwa kutumia silaha kuwa sasa mwisho wao umefika kwani jeshi lake sasa halilali kuhakikisha kuwa wanatiwa ndani ya mikono ya polisi.kamishna kova ameyasema hayo leo mchana wakati akizungumza na wanahabari ofisini kwake .

Bastola zaidi ya tano ambazo zilikuwa mikononi mwa wahalifu ambapo polisi kanda maalum wamefanikiwa kuzitia mikononi,jitihada zinaendelea kuhakikisha jiji linakuwa salama
KATIKA HATUA NYINGINE----
JESHI la polisi kanda maalum  jijini Dar es salaam linamshikilia SIMON
MEENA (40)mkazi wa Kinyerezi  Segerea kwatuhuma za kuwasumbua wafanyabiashara mbalimbali  mjini hapa kwa kuwa kuwasingizia pamoja nakuwatuhumu kwamba wanahusika na makosa  yenye kuhatarisha usalama .

HILI NDILO JAMBO WALILOFANYA YANGA NA CRDB LEO

 Uongozi wa klabu ya Young Africans leo umewekeana sahihi ya makubaliano na Benki ya CRDB nchini juu ya uboreshaji na utengenezaji wa kadi za uanachama, hafla hiyo imefanyika katika Makao Makuu ya Benki hiyo eneo la Posta mpya jijni Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Dr Charles Kimei amesema anaushukuru uongozi wa Yanga kwa kuwaamini benki yao kuwa wanaweza kufanya kazi hiyo, na sisi tunaamini tutafanya kazi vizuri na kuweza kufikia malengo yao waliyotuwekea katika kipindi muafaka.
Kwetu sie kupata nafasi ya kufanya kazi na klabu ya Yanga ni jambo jema, tunatambua wana wana wapenzi zaidi ya milioni 20 nchi nzima, hivyo ni jukumu letu kuhakikisha tunawifikia kila sehemu walipo na wanajiunga na uanachama wa kalbu yao pendwa alisema “Dr Kimei”.
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB, Dr Charles Kimei (kulia), akibadilishana mkataba  mjumbe wa bodi ya Wadhamini Bi Fatma Karume (katikaki), kushoto ni makamu mwenyekiti wa Yanga Bw Clement Sanga
Aidha Kimei amesema kwa utaratibu huo wa mfumo wa kisasa, wataanza kwa kutoa bure kadi za uanchama wa Yanga ambazo zitakua na nembo ya VISA itakayomfanya mtumiaji aweze kuitumia sehem yoyote alipo na kurahisisha zoezi la ukusanyaji wa ada za uanachama.

TIGO IMETISHA--SASA WATEJA WA TIGO PESA WANAGAIWA FAIDA ,SOMA UONE

Meneja mkuu wa Tigo Tanzania DIEGO GUTIERREZ akizungumza na wanahabari mapema leo juu ya huduma hiyo  
 Kampuni ya mawasiliano ya TIGO Tanzania leo imetangaza kutoa gawio la kiasi cha shilingi billion 14.25 sawa na dola za kimarekani 8.7 lililolimbikizwa katika account  yake ya fedha ya tigo pesa kwa ajili ya wateja wake.hii inafanya kampuni hiyo kuwa mtandao wa kwanza wa simu duniani kutoa gawio la fedha kutokana na huduma ya kutuma na kutoa fedha.
       Acount ya mfuko wa fedha wa tigo pesa TIGO PESA TRUST ACCOUNT ni account ambayo fedha za tigo pesa zinakusanywa na kuhifadhiwa toka huduma ya tigo pesa ilipoanza miaka minne iliyopita.Kwa sasa TIGO  ipo tayari kutoa gawio la fedha hizo ambazo zilikuwa zinazaa faida baada ya kuridhiwa na benk kuu ya Tanzania BOT kwa barua rasmi ya kutokuwa na pingamizi iliyopokelewa julai mwaka huu.
       Akizungumza na wanahabari leo meneja mkuu wa TIGO Tanzania  DIEGO GUTIERREZ amesema kuwa gawio hilo la faida litawanufaisha wateja wote wa tigo wakiwemo mawakala wakuu mawakala wa reja reja na mteja mmoja mmoja mtumiaji wa tigo pesa.
Amesema kuwa kwa miaka mitatu na nusu sasa mfuko wa fedha wa tigo pesa ulikuwa ukikusanya faida  ya kiwango cha asilimia 5 hadi 12 na mpaka juni mwaka huu faida hiyo imefikia shilingi billion 14.25 na kuongeza kuwa lengo ni kuwapatia wadau wa tigo fursa ya kupata faida kutokana na kiasi cha fedha walichoweza kukiweka katika account zao za tigo pesa.
Aidha amesema kuwa wastani wa faida ambayo mteja yeyote ataweza kupata inatofautiana na wastani wa fedha ambayo ataweza kubaki nayo kwenye account yake ya tigo pesa kwa siku kwa hiyo viwango vinatofautiana kati ya wakala mkuu,wakala wa rejareja na mteja mmoja mmoja.


Gawio hilo litawanufaisha zaidi ya wateja million 3.5 wa tigo pesa nchini wakiwemo mawakala wakuu,mawakala wa reja reja.

Monday, September 1, 2014

michezo--PICHA TATU ZA CHICHARITO AKITAMBULISHWA REAL MADRID MUDA HUU

Rais wa Real Madrid, Florentino Perez akimkabidhi jezi mshambuliaji mpya, Javier Hernandez 'Chicharito' aliyetua kwa mkopo kutoka Manchester United leo.

STORY NZIMA YA MGOMO WA WAFANYABIASHARA HAPA KARIAKOO IPO HAPA LIVE

Na Karoli Vinsent


      SIKU moja kupita baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kutoa onyo kwa wafanyabiashara juu ya uhakiki wa mashine za Kielektroniki EFDs, wafanyabiashara wa maduka Kariakoo wamegoma kufungua maduka  huku wakiishinikiza serikali kuwapunguzia kodi.


          Wafanyabiashara hao walifikia hatua hiyo, baada ya kupata taarifa kutoka TRA ya kwamba watafanyiwa ukaguzi endelevu na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa wale watakaokutwa hawatumii mashine hizo na wale wanaohamasisha kuwarubuni wengine wasitumie mashine hizo.

MAKOMANDO WA NEPAL WAONYESHA KAMPUNI ILIYOWALETA,TIZAMA HAPA

Komando kutoka nchini NEPAL,SHIDHEE BAHADURKATUWAL akionyesha nyumba ya mnyarwanda aliyokuwa akiilinda kupitia kampuni ya ADVANCED SECURITY  karibu na uwanja wandege wa mwalimu nyerere jijini Dar es salaam

Maafisa wa uhamiaji Dar es salaam wakimhoji mama wa kitanzania ambaye ameolewa na mnyarwanda huyo ambao kwa pamoja nyumba yao ilikuwa ikilindwa na makomando hao kutoka jeshi la nchi ya NEPAL

Hapa wakiwa ndani ya sare zao za kazi za kampuni hiyo ya ulinzi ya ADVANCED SECURITY ambayo inatuhumiwa kuwaingiza wanajeshi hao wa jeshi la NEPAL kinyume na sheria kwa lengo la kuwapatia kazi za ulinzi nchini 


michezo--FALCAO ATUA MAN UNITED

Manchester United wameshinda mbio na kumnyakuwa Radamel Falcao kwa mkopo kutoka Monaco.
Manchester United wameshinda mbio na kumnyakuwa Radamel Falcao kwa mkopo kutoka Monaco.
Manchester United wameshinda kinyang’anyiro cha kumsajili Radamel Falcao kutoka Monaco kwa mkopo kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Mshambuliaji huyo ataigharimu Old Trafford pauni milioni 12, akiungana na Angel Di Maria, Dalley Blind, Luke Shaw, Ander Herrera na Marcos Rojo waliojiunga na kocha Louis van Gaal klabuni hapo.
Raia huyo wa Colombia, 28 amekubaliana na masharti binafsi – na inaripotiwa kuwa atalipwa pauni 200,000 kwa wiki huku ikiaminika akiwa njiani kwenda Manchester kwa ndege binafsi.

LIVE KUTOKA HAPA KARIAKOO--WAMEGOMA TENA

Wafanya biashara wa maduka katika soko la kariakoo jijini Dar es salaam leo wameamua kufunga maduka yao ikiwa ni sehemu ya kile ambacho kinatajwa kuwa ni mgomo wao wa kimya kimya ambao umeanza leo.
Mwandishi wa mtandao huu hadi sasa ameweka kambi katika soko hilo na hadi sasa sehemu kubwa ya soko hili maduka yake yamefungwa na huku wafanya biashara hao wakiwa hawapo kabisa katika maduka hayo.
Chanzo cha mgomo huu bado hakijawekwa wazi na wahusika hao ila habari zinasema kuwa ni mwendelezo wa migomo yao ya kupinga matumizi ya mashine za kielectronic za EFD.
HABARI ZAIDI ZITAKUJIA HAPA 
Huu ndio monekano wa soko la Kariakoo kwa sasa huku wateja mbalimbali wakiwa hawana la kufanya kutokana na maduka mengi kufungwa na kukosa huduma